Saturday, February 11, 2017

Arsenal 2 - 0 Hull City, Sanchez ampa usingizi Wenger


Mchezo mmoja wakamilika huko Emirates Stadium na wenyeji Arsenal wameibuka na ushindi  wa 2 – 0 kwa magoli ya Alexis Sanchez katika dakika 34 na 90(p).

Dakika ya 34 kazi nzuri ya Mesut Oezil iliokolewa na kumkuta Kieran Gibbs ambae nae aliuelekeza mpira kimiani ila uhodari wa kipa aliweza kuokoa mchomo huo na kumkuta Alexis Sanchez aliepiga tena ukaokolewa na kumbabatiza mkononi na kuingia wavuni,

Goli la pili lilitokana na mpira wa penati ambayo mchezaji wa Hully City Sam Clucas aliunawa kwa makusudi mpira uliopigwa na Lucas Perez, na mwamuzi alimpa kadi nyekundu ya moja kwa moja na penati ilipigwa na Sanchez na kuipatia timu yake uongozi wa 2 – 0.

Arsenal sasa imefikisha pointi 50 sawa na totenham iliyo nafasi ya pili ila imezidiwa idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa.

Mpka mwisho wa mchezo huo Arsenal 2 – 0 Hull City na kuzima ngebe za hull city kuvitesa vilabu vikubwa.
kadi
 Arsenal: Theo Walcott 53’ (Y), Kieran Gibbs 55’(Y) Alexis Sanchez 76’(Y)

Hull City:  Andrea Ranocchia 70’(Y) Sam Clucas 90’(R)

0 comments:

Post a Comment