Sunday, June 12, 2016

USAJILI SIMBA NI TISHIO

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Pope ametamba kuwa wamejipanga kufanya usajili wa kisayansi zaidi lengo likiwa ni kupata kikosi imara kitakachowapa ubingwa msimu ujao.

Kwa miaka mitatu mfululizo Simba hawajabeba ubingwa wa ligi kuu sababu ikisemwa kuwa ni usajili mbovu. Hans Pope amekiri kuwa wamejifunza mambo mengi katika kipindi hiki ambacho timu ilikuwa haifanyi vizuri na sasa wapo tayari kufanya mambo makubwa kutokana na usajili wao watakaoufanya. Hans Pope aliweka kambi nchini Zimbabwe akisaka wachezaji watakaoleta raha kwa mashabiki wa Simba msimu ujao.

"Simba tumepita katika wakati mgumu ukiwemo kutukanwa na kudhalilishwa kutokana na mwenendo mbaya wa timu, ukweli tumekubaliana msimu uliopita uwe mwisho na msimu ujao uwe wa vitendo" alisema Hans Pope.

"Ndio maana hivi sasa tutapambana huku na kule kutafuta kocha na wachezaji ambao watairudisha timu kama ilivyokuwa siku za nyuma." aliongeza Hans Pope ambaye aliwahi kuzingirwa na mashabiki wa Simba wakimtaka atoke katika klabu hiyo kutokana na matokeo mabaya waliyokuwa wanayapata msimu uliopita.

Hans Pope alisema Hamisi Kiiza alianza vizuri katika klabu hiyo, lakini baada ya kusifiwa alianza kuringa na kuiweka timu katika wakati mgumu na hiyo ilitokana na kukosa mtu sahihi wa kucheza nafasi yake.

Related Posts:

  • HAWA NDO WANAOTUPIWA VIRAGO KLABU YA SIMBA Simba ipo katika harakati za kukisuka upya kikosi chao na tayari taarifa za ndani ya klabu hiyo zimeonyesha wazi wachezaji ambao wataondoka klabuni hapo kupisha wengine waendeleze gurudumu Msimbazi. Kwa mujibu wa Gazeti … Read More
  • KLABU 2 ZA MISRI VITANI KUWANIA SAINI YA DONALD NGOMA Klabu za Misri Al Ahly na Zamalek zipo katika vita ya kuwania saini ya Mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma. Uwezo mkubwa wa Donald Ngoma anapokuwa uwanjani umezifanya klabu nyingi kuhitaji saini ya mchezaji huyo anaeitumi… Read More
  • JOSE MOURINHO ATANGAZWA RASMI KUWA KOCHA WA MANCHESTER UNITED JOSE MOURINHO ametangazwa rasmi kuwa kocha mkuu wa Manchester United kwa mkataba wa miaka 3. Mourinho amechukua mikoba ya Louis Van Gaal na anakuwa kocha wa 25 kwa United. Hii hapa ni tweet ya akaunti rasmi ya Machester … Read More
  • PAUL NONGA ANYOOSHA MIKONO YANGA Mchezaji aliyejiunga na Yanga akitokea Stand United Paul Nonga amesema ameuomba uongozi wa Yanga umuuze. Nonga amefikia uamuzi huo baada ya kukosa nafasi ya kucheza muda mwingi katika klabu hiyo. ”Nimeomba kuuzwa na tay… Read More
  • AL AHLY WAMNYATIA DONALD NGOMA Mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe Donald Ngoma ameanza kuwindwana vigogo wa soka la Misri na Afria timu ya Al Ahly. Ngoma amekuwa mshambuliaji tishio sana katika klabu ya Yanga na ametoa mchango mkubwa sana katika ma… Read More

0 comments:

Post a Comment