Sunday, June 12, 2016

KIPA YANGA ASAKA KLABU YA KUHAMIA

Baada ya Yanga kufanikiwa kumsajili mlinda mlango kutoka timu ya Tanzania Prisons, Ben Kakolanya, Mlinda mlango wa siku nyingi wa klabu hiyo, Benedictor Tinoco amesema ni wakati wake kuangalia sehemu gani atacheza msimu ujao.

Usajili wa Kakolanya unawafanya Yanga kuwa na magolikipa wanne ambao ni Ally Mustafa, Deogratius Munish, Kakolanya pamoja na Benedictor Tinoco, Tinoco tangu asajiliwe msimu uuliopita akitokea Kagera Sugar hajapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza.

Mkataba wake na klabu ya Yanga haujaisha lakini ujio wa kipa mpya kikosini hapo unaonyesha wazi kuwa anahitaji kwenda kujaribu sehemu nyingine ili kulinda kiwango chake kisishuke.

"Siwezi kukaa Yanga milele, nahitaji kuangalia mbele na kutafuta timu ambayo itanisaidia kulinda kiwango changu na kutimiza ndoto zangu" alisema Tinoco.

Tinoco anatamani kupata timu ambayo ataweza kucheza kwani yeye mwenyewe anaamini uwezo anao mkubwa isipokuwa hakuwahi kupata nafasi ya kuonyesha kipaji chake Yanga.

Ushindani uliopo katika klabu ya Yanga umefanya idadi ya wachezaji wanaoomba kuondoka klabuni hapo kufikia watatu sasa, baada ya Paul Nonga kuandika barua kwa uongozi wa timu hiyo akiomba wamuuze, Malimi Busungu nae ametajwa kuomba kwenda kujiunga Stand United ili kulinda kiwango chake pamoja na Tinoco ambaye anahofia nafasi yake Jangwani kwa sasa.

Related Posts:

  • CAF YAISAFISHIA NJIA YANGAShirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF), limemthibitisha beki Hassan Kessy kuichezea Yanga katika michuano ya Kombe la CAF CC katika hatua ya makundi. Caf pia imetuma leseni ya wachezaji wengine watatu wa Yanga walioonge… Read More
  • MATARAJIO YA SIMBA KIKOSI KIPYA MSIMU UJAOZacharia Hans Poppe, mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba, amesem a kikosi chao msimu ujao kitakuwa na mabadiliko makubwa kuanzia benchi la ufundi hadi wachezaji. Simba kwa sasa ipo katika harakati za kuhakikisha wanawana… Read More
  • KIFAA KIPYA YANGA KUTUA LEO JANGWANIWalter Musona Mshambuliaji kutoka FC Platinum ya Zimbabwe anatarajiw kuwasili Daresalaam leo alasiri kwa ajili ya mazungumzo na klabu ya Yanga. Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka katika klabu ya Yanga, tayari mambo yo… Read More
  • STAND UNITED YAISHITAKI SHIREFA TFFUongozi wa Stand United, umeliomba shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF kukemea kitendo cha uongozi wa chama cha soka Mkoani Shinyanga (SHIREFA) kuandikisha wanachama wa klabu hiyo wakati kuna viongozi. Mwenyekiti wa … Read More
  • KASEKE ACHEKELEA MAISHA YANGAKiungo wa Yanga, Deus Kaseke amesema anajiona ni mwenye bahati kwa kufanikiwa kuchukua mataji mawili (Ligi kuu Vodacom & Kombe la FA) pamoja na kucheza hatua ya makundi kombe la shirikisho Afrika CAF CC katika msimu wake … Read More

0 comments:

Post a Comment