Sunday, June 12, 2016

HUYU MWINGINE ALIYENASWA NA WEKUNDU WA MSIMBAZI

Simba imemsainisha beki wa Mwadui Emmanuel Semwanza.

Semwanza ameichezea Mwadui kwenye mzunguko wa pili baada ya kununuliwa kwenye kipindi cha usajili wa dirisha dogo akitokea African Lyon, tayari Beki huyo amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba Juzi Alhamisi majira ya saa 5 Usiku.

"Usiku huu tumefanikiwa kumsainisha Semwanza (Emmanuel) kutoka Mwadui ambaye ni miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa kwenye orodha yetu. Bado kuna sura nyingine za kazi zinakuja hivyo wapenzi wetu wasiwe na wasiwasi" yalisemwa na kiongozi wa Simba.

Beki huyo nae baada ya kusajiliwa na klabu ya Simba alisema kwa muda mrefu alikuwa na ndoto za kuichezea Simba na hivyo anafuraha kwa kujiunga na wekundu hao wa msimbazi.

"Kwa Muda mrefu nilikuwa na hamu ya kuichezea Simba na nadhani hawajakosea kunisajili. Nataka kuthibitisha uwezo wangu na kuisaidia Simba ifanye vizuri." alisema Semwanza.

Aidha beki huyo aliwashukuru viongozi wa Mwadui kwa ushirikiano waliompa kipindi anaitumikia klabu hiyo na kuwataka watambue kuwa kujiunga kwake Simba ni nafasi kwake kuendeleza kipaji chake katika soka.

Related Posts:

  • USAJILI SIMBA NI TISHIOMwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Pope ametamba kuwa wamejipanga kufanya usajili wa kisayansi zaidi lengo likiwa ni kupata kikosi imara kitakachowapa ubingwa msimu ujao. Kwa miaka mitatu mful… Read More
  • YANGA YATUMA MAJINA YA NYOTA WAO WAPYA CAFKlabu ya Yanga imewasilisha majina ya wachezaji wake CAF waliowasajili hivi karibuni ambao ni Hassan Ramadhan Kessy, Juma Mahadhi, Vicent Andrew na Beno Kakolanya kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo katika kombe la shirikisho … Read More
  • SIMBA YAMNASA WINGA MACHACHARI, ASAINI MIAKA 2 Klabu ya Simba Sports Club imefanikiwa kumsajili mchezaji wa Mwadui FC, Jamali Mnyate aliyesaini mkataba wa miaka 2 kwa uhamisho wa Tsh. Milioni 15. Kufuatia usajili huo Makamu Rais wa klabu hiyo, Geofrey Nyange Kaburu a… Read More
  • JUMA ABDUL, SALUM TELELA KUWAKOSA WAALGERIAWachezaji Juma Abdul na Salum Telela wataikosa mechi kati ya Yanga na Mo Bejaia, mechi ya kwanza katika hatua ya makundi kombe la shirikisho CAF. Telela na Juma Abdul hawatakuwepo katika kikosi kitakachoenda nchini Uturuki… Read More
  • KIPA YANGA ASAKA KLABU YA KUHAMIABaada ya Yanga kufanikiwa kumsajili mlinda mlango kutoka timu ya Tanzania Prisons, Ben Kakolanya, Mlinda mlango wa siku nyingi wa klabu hiyo, Benedictor Tinoco amesema ni wakati wake kuangalia sehemu gani atacheza msimu ujao.… Read More

0 comments:

Post a Comment