Sunday, June 12, 2016

JUMA ABDUL, SALUM TELELA KUWAKOSA WAALGERIA

Wachezaji Juma Abdul na Salum Telela wataikosa mechi kati ya Yanga na Mo Bejaia, mechi ya kwanza katika hatua ya makundi kombe la shirikisho CAF.

Telela na Juma Abdul hawatakuwepo katika kikosi kitakachoenda nchini Uturuki kwa kambi ya siku Tano kujiandaa na mchezo wao wa kombe la shirikisho la soka Afrika (CAF CC) dhidi ya Mo Bejaia ya nchini Algeria. Kwa mujibu wa Meneja wa Yanga Hafidh Saleh, Juma Abdul ataikosa mechi hiyo kwa sababu ni majeruhi wakati Telela yeye mkataba wake umemalizika klabuni hapo na uongozi wa timu mpaka sasa haujamuongezea mkataba mpya.

"Juma Abdul ni majeruhi, hivyo hatoweza kwenda, Telela yeye mkataba wake umeisha na mpaka sasa uongozi bado haujamuongezea" alisema Hafidh Saleh.

Aidha wachezaji wapya wa timu hiyo, ambao ni Hassan Kessy, Andrew Vicent, Juma Mahadhi na Beno Kakolanya watakuwa ni miongoni mwa watakaokuwepo katika msafara huo.

Inadaiwa kuwa Telela ameshafanya mazungumzo na timu za Simba na Azam kwa nia ya kumsajili kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.

Saleh amesema mara baada ya mchezo wao na MO Bejaia watarejea Uturuki kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo utakaofanyika uwanja wa Taifa, Dar Es Salaam na watarejea nchini siki mbili kabla ya mchezo huo.

Related Posts:

  • BAADA YA KUTUPIWA VIRAGO HAMISI KIIZA AICHANA VIBAYA SIMBA Hamisi Kiiza ambaye aliingia katika mgogoro na uongozi wa timu yake ya zamani ya Simba SC ameamua kufunguka na kusema kwamba timu hiyo hata isajili nyota wote kamwe haitafanikiwa. Kiiza aliyeshika nafasi ya pili kwa upach… Read More
  • YANAYOJIRI KATIKA KILELE CHA SIMBA DAY LEO TAIFA Mashabiki Wakionekana Wenye Furaha Tele Keki Yenyewe ya Simba Day Hii Hapa Twanga Pepeta Wakiwa tayari wameshawasili Uwanja wa taifa kutoa burudani Mashabiki Wakishangilia Sherehe hizo za Simba DayUngana na Sok… Read More
  • YALIYOJIRI MKUTANO MKUU WA DHARULA YANGA Katika mkutano mkuu wa dharula wa klabu ya Yanga uliofanyika leo ukumbi wa Diamond Jubilee, Mwenyekiti Yusuf Manji ameomba apewe klabu kwa miaka 10 na katika kipindi hicho atakuwa anachukua asilimia 75 ya mapato ya timu, huk… Read More
  • AZAM FC YANASA WENGINE WAWILI KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo jioni imeingia mkataba na mabeki wawili, Mghana Daniel Amoah na Mzimbabwe, Bruce Kangwa, kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo msimu ujao. Wawili hao kila mmoja amesaini m… Read More
  • MWASHIUYA KUIKOSA MEDEAMA SC GHANA Kiungo klabu ya Yanga, Geofry Mwashiuya ataukosa mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Medeama SC utakaopigwa nchini Ghana kutokana kuuguza majeraha ya goti. Mwashiuya amewekewa bandeji laini ambayo inamsaidia kupona hara… Read More

0 comments:

Post a Comment