Sunday, June 12, 2016

YANGA YATUMA MAJINA YA NYOTA WAO WAPYA CAF

Klabu ya Yanga imewasilisha majina ya wachezaji wake CAF waliowasajili hivi karibuni ambao ni Hassan Ramadhan Kessy, Juma Mahadhi, Vicent Andrew na Beno Kakolanya kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo katika kombe la shirikisho Afrika CAF.

Hans amesema ameridhika na viwango vya wachezaji hao kutokana na kile walichokionyesha kwenye mazoezi ya timu.

"Nimeridhika kabisa na uwezo waliouonyesha kwenye mazoezi ya siku mbili tatu ndiyo maana tukayatuma majina yao nikiamini watakuwa na msaada kwetu hasa kutokana wamekuja kwenye timu ya ushindi" alisema Pluijm.

Yanga sasa imebakisha nafasi mbili ili kujaza kikosi chao baada ya kuwanasa hao wanne.
Mechi ya kwanza ya hatua hiyo ya makundi Yanga itacheza na MO Bejaia ya nchini Algeria, mchezo utakaopigwa huko nchini Algeria tarehe 19, Juni, 2016.

Related Posts:

  • JKT OLJORO YAMIMINIWA MAMILIONITimu ya maafande wa JKT Oljoro ya jijini Arusha inayojiandaa na michuano ya ligi daraja la pili (SDL) msimu wa 2016/17 imekabidhiwa vifaa vya michezo vyenye thamani ya Shi. Milioni 3.4 kutoka kwa kampuni ya Sanlam. Vifaa h… Read More
  • KAPOMBE,WAWA WATUA SAUZI KWA UCHUNGUZINYOTA wawili wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Shomari Kapombe na Pascal Wawa hivi sasa wapo jijini Cape Town, Afrika Kusini kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya zao. Mabeki hao waliondoka nchini tok… Read More
  • HATIMAYE TAMBWE AFUNGUKA UJIO WA CHIRWA YANGAMshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe amesema kucheza timu kubwa kama Yanga kunahitaji ujasiri kutokana na usajili unaofanywa kila wakati. Ujio wa mshambuliaji mpya kwenye kikosi cha Yanga, Mzambia Obrey Chirwa, unaonekana … Read More
  • SIMBA YAPEWA SOMOMwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Ismail Rage ameutaka uongozi wa Simba uliopo madarakani kuacha malumbano na wachezaji. Kumekuwa na kutokuelewana kwa siku za hivi karibuni baina ya wachezaji na viongozi wa Simba kit… Read More
  • KIBARUA CHA LAURENT BLANC CHAOTA NYASI PSGKlabu ya PSG imemtimua kocha wake Laurent Blanc, kwa mujibu wa jarida la la L'Equipe la nchini Ufaransa. Taarifa za kutimuliwa kwa kocha huyo bado hazijawa rasmi kwani mpaka hivi sasa klabu ya PSG haijatoa tamko rasmi laki… Read More

0 comments:

Post a Comment