Wednesday, May 18, 2016

RATIBA YA FAINALI KOMBE LA FA YABADILISHWA


Fainali za kuwania Kombe la Shirikisho maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) zitakazokutanisha timu za soka ya Young Africans na Azam FC, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa zitafanyika Mei 25, 2016 kama ilivyotangazwa awali.

Awali fainali hizo zilipangwa Juni 11, 2016 ili kuzipa muda wa kuajindaa timu mara baada ya michezo ya mwisho ya Ligi Kuu ya Vodacom inayotarajiwa kufikia ukomo Mei 22, 2016, lakini imeachwa tarehe ya awali ili kuenenda na kanuni ya tarehe ya mashindano kwani mwisho wa msimu ni Mei 31, mwaka huu.

Kadhalika tarehe ya awali ilipangwa kutokana ratiba kubana hasa ya timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ambayo ina mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Kenya ‘Harambee Stars’ unaotarajiwa kufanyika Mei 29, mwaka huu. Mchezo huo unaingia kwenye kalenda ya FIFA.

Taifa Stars itacheza mechi hiyo ikiwa ni maandalizi ya mchezo wake dhidi ya Misri unaotarajiwa kufanyika Juni 4, 2016 jijini Dar es Salaam kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).

Tayari TFF imefafanua iwapo Bingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa msimu 2015/16 inayoendelea atashinda pia taji katika fainali za Kombe la Shirikisho la ASFC, ndiye atayeiwakilisha nchi katika michuano ya Ligi ya mabingwa wa Afrika msimu wa 2016/17.

Kwa msingi huo, timu itayopoteza fungwa katika fainali hizo za Kombe la Shirikisho –ASFC linalodhaminiwa na kituo cha Televisheni cha Azam, ndiyo itakayowakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika katika msimu wa 2016/17

Fainali za Kombe la Shirikisho zinakuja baada ya mchuano ulioshindanisha timu 64 za Ligi Kuu Tanzania Bara - VPL (16); Ligi Daraja la Kwanza -FDL (24), Ligi Daraja la Pili – SDL (24) 

Related Posts:

  • PLUIJM:"YANGA TIMU BORA TANZANIA" Kocha wa Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Hans Van Pluijm amesema Yanga bado ni timu bora zaidi Tanzania Licha ya kuondolewa katika michuano ya kimataifa. Yanga imetupwa nje ya michuano ya kombe la shirikisho … Read More
  • SIMBA YABADILI GIA ANGANI Sare ya bila kufunguna waliyoipata Simba dhidi ya JKT Ruvu imemfanya kocha wa klabu hiyo, Joseph Omog kubadili mfumo wa uchezaji na kusisitiza umakini kwa wachezaji katika mechi zijazo. Katika mchezo huo dhidi ya JKT Ruvu… Read More
  • OMOG ASHUSHA PRESHA ZA WANAMSIMBAZI Kocha wa klabu ya Simba, Mcameroon, Joseph Omog amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa watulivu kufuatia sare ya bila kufungana waliyoipata dhidi ya JKT Ruvu. Omog amesema hayo ni matokeo ya kawaida ya kimchezo hivyo mash… Read More
  • BOCCO AITISHIA NYAU SIMBA ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya kupambana na Simba, Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’, amesema kuwa wanamorali kubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo utakaofanyika … Read More
  • TANZIA;BABA YAKE DEOGRATIUS MUNISH "DIDA" AAGA DUNIABaba wa Mlinda Mlango namba 1 wa Mabingwa Watetezi wa Ligi kuu Tanzania Bara, Deogratius Munish amefariki Dunia mchana wa leo. Mzee Munishi ameaga dunia mchana wa leo, kifo chake kimetokea wakati tayari Dida anakaribia kuingi… Read More

0 comments:

Post a Comment