Thursday, July 21, 2016

YANGA WAMWONGEZEA MKATABA PLUIJM

Mabingwa wa ligi kuu Vodacom na wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC), Yanga wamemwongezea mkatabawa miaka miwili kocha wao Hans Van Pluijm.

Kocha huyo ambaye ameipa mafanikio makubwa klabu ya Yanga ikiwemo kufikisha katika hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika alisema anaipenda sana klabu ya Yanga na kwamba anajitahidi kila uchao kuhakikisha analeta heshima na furaha kwa viongozi, wanachama na mashabiki wa klabu hiyo.

“Naipenda hii klabu sikuzote nimekuwa nikifanya kazi kwa kutanguliza heshima na mapenzi ambayo watu wa Yanga wamekuwa wakinionyesha, sasa nimeongeza mkataba ambao hata familia yangu ina furaha na hilo,” amesema Pluijm

Aidha Pluijm aliongeza kuwa anachangamoto kubwa sana katika kuhakikisha Yanga inaendelea kufanya vizuri zaidi ya walipofikia mwaka huu huku akiweka wazi kuwa anajua ni kazi ngumu lakini atapambana ili kufikia malengo.

“Changamoto yangu kubwa sasa ni kuhakikisha Yanga inafanya mazuri zaidi kuzidi ya haya tuliyoyapata msimu huu najua haitakuwa kazi rahisi lakini hakuna namna lazima tupambane kila mmoja na nafasi yake kuweza kufikia malengo.”
Ungana Na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA  Kwa Habari Za Haraka Za Soka Kote Ulimwenguni.

Related Posts:

  • MAN U WAANZA KUUZA JEZI NA. 9 YA IBRAHIMOVIC Kwa mujibu wa ripoti zilizoenea sana siku za hivi karibuni ni kwamba Zlatan Ibrahimovic anakaribia kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Man U. Tangu aondoke PSG kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu wa 2015/16, Zlatan… Read More
  • JAMES RODRIGUEZ AITAJA KLABU ANAYOTAKA KUHAMIA James Rodriguez amesema anataka kujiunga na wababe wa soka la Ufaransa klabu ya Paris Saint-Germain msimu ujao. Rodriguez alikuwa akihusishwa sana kutimkia ligi kuu ya Uingereza lakini amesema anatamani kujiunga na PSG. … Read More
  • CHELSEA YATHIBITISHA KUMSAJILI MCHEZAJI HUYU Klabu ya Chelsea imetangaza kumsajili Juan Familia-Castillo akitokea klabu ya Ajax. Kila mwaka Chelsea inawapandisha vijana kutoka katika kikosi chao cha vijana na mwaka huu tayari Castillo amepata bahati hiyo kutokana… Read More
  • ONYO KALI NA MUHIMU KWA YANGA KUELEKEA MECHI YAO LEOMwenyekiti wa zamani wa Simba Ismail Aden Rage amesema wachezaji wapya waliosajiliwa Yanga hawana leseni za kuichezea timu hiyo katika mchezo wa leo. Rage amesema Sheria ya Usajili ya michuano ya Kombe la shirikisho namba … Read More
  • RASMI:DANI ALVES ATUA JUVENTUSMchezaji wa kimataifa wa Brazil, Dani Alves ametua katika klabu ya Juventus akitokea Barcelona. Dani Alves amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Juventus akitokea Barcelona na kusaini mkataba wa miaka miwili na mabingw… Read More

0 comments:

Post a Comment