Thursday, July 21, 2016

PICHA ALIYOPOST MKEWE MOURINHO YAZUA UTATA UJIO WA POGBA MAN U

Mashabiki wa Manchester United wamekuwa katika hali ya sintofahamu kuhusu ujio wa Pogba Man U hasa baada ya Mke wa Jose Mourinho kupost picha ambayo Mourinho amemjumuisha Pogba katika hesabu zake.


Picha hiyo ilipostiwa katika mtandao wa twiter na mke huyo wa Mourinho ikionyesha ubao ambao makocha huutumia katika kupanga mbinu zao. Katika picha hiyo katikati panaonekana jina la Pogba na Fellaini wakati huo suala la Pogba kutua Man U bado likiwa ni kitendawili.

Ukiangalia kwa makini sehemu iliyozungushiwa ranig nyekundu kwa juu linaonekana jina la Pogba na chini yake lipo la Fellaini
Picha hiyo pia inayonyesha kuwepo katika ofisi ya Mourinho, Mashabiki waliamua kuikuza (Zoom) picha hiyo na kufanikiwa kuliona jina la Pogba katika ubao huo.
Ungana Na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA  Kwa Habari Za Haraka Za Soka Kote Ulimwenguni.





0 comments:

Post a Comment