Thursday, June 9, 2016

TFF YATANGAZA TAREHE YA KUFUNGULIWA DIRISHA LA USAJILI

Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania TFF limetangaza tarehe ya kuanza kwa zoezi la usajili kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu Vodacom Tanzania kuwa ni Juni 15 hadi Agosti 6, 2016.


Kwa mujibu wa kalenda ya shirikisho hilo, usajili utaanza rasmi Juni 15 na kufungwa Julai 30, 2016.
Kuanzia Juni 15 hadi Julai 30 timu zote zinazoshiriki ligi kuu Vodacom zitatumia kutangaza wachezaji wanaowaacha na kusajili wapya.

Pingamizi itakuwa Agosti 7 hadi 14, 2016, uthibitishwaji wa usajili hatua ya kwanza ni kati ya Agosti 15 na Agosti 19.

Usajili hatua ya pili ni Agosti 17 hadi Septemba 7, 2016 na kipindi cha pingamizi hatua ya pili ni kuanzia Septemba 8 hadi Septemba 14.

Septemba 15 hadi Septemba 17 ni kipindi cha kuthibitisha usajili hatua ya pili.

Timu zimetakiwa kuanza maadalizi kuanzia Juni 15 hadi Julai 15, 2016 na kuanzia Julai 16, 2016 hadi Agosti 14 ni kipindi cha mechi za kirafiki za ndani na nje.

Ratiba ya Ligi kuu Vodacom msimu ujao wa 2016/17 inatarajiwa kutoka kati ya Julai 16 hadi Agosti 14, 2016.

Related Posts:

  • BOCCO AITISHIA NYAU SIMBA ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya kupambana na Simba, Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’, amesema kuwa wanamorali kubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo utakaofanyika … Read More
  • AZAM FC YANASA WENGINE WAWILI KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo jioni imeingia mkataba na mabeki wawili, Mghana Daniel Amoah na Mzimbabwe, Bruce Kangwa, kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo msimu ujao. Wawili hao kila mmoja amesaini m… Read More
  • SIMBA YABADILI GIA ANGANI Sare ya bila kufunguna waliyoipata Simba dhidi ya JKT Ruvu imemfanya kocha wa klabu hiyo, Joseph Omog kubadili mfumo wa uchezaji na kusisitiza umakini kwa wachezaji katika mechi zijazo. Katika mchezo huo dhidi ya JKT Ruvu… Read More
  • OMOG ASHUSHA PRESHA ZA WANAMSIMBAZI Kocha wa klabu ya Simba, Mcameroon, Joseph Omog amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa watulivu kufuatia sare ya bila kufungana waliyoipata dhidi ya JKT Ruvu. Omog amesema hayo ni matokeo ya kawaida ya kimchezo hivyo mash… Read More
  • SIMBA WAIPANIA NDANDA FC Katibu mkuu wa Simba, Patrick kahemela ameapa kurudisha furaha na kuachana na machungu ya kutoka vichwa chini katika mechi zao za ligi kuu. Kiongozi huyo amesema Ndanda FC ndiyo itakuwa ya mfano kwani imepania kuwapa raha… Read More

0 comments:

Post a Comment