Mchakato wa Azam Fc kusaka mchezaji bora wa timu hiyo umemalizika hivi karibuni na Shomari Kapombe kuibuka mshindi wa tuzo hizo.
Azam Fc imetoa tuzo kwa wachezaji wake wanne waliopata kura nyingi kutokana na msaada wao katika timu hiyo uliousaidia Azam Fc kumaliza katika nafasi ya pili ligi kuu Vodacom msimu wa 2015/16.
Shomari Kapombe ndiye aliyeibuka kinara kwa kujikusanyia kura 277 akifuatiwa na kipa Aishi Manula aliyepata kura 120, Pascal Wawa nafasi ya tatu kwa kura 40 na nafasi ya nne imeenda kwa kiungo mkabaji Himid Mao aliyejipatia kura 30.
Mtendaji mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba amesema huo ni utaratibu ambao wamejiwekea kwa lengo la kuwaongezea hamasa ya kujituma wachezaji wao ili kuongeza ushindani na kupata mafanikio.
"Tutatoa zawadi kwa kila mshindi zawadi ambayo itakuwa kubwa lengo ni kuamsha ari na kuongeza ushindani kwa wachezaji wetu ili tuweze kufanya vizuri katika mashindano tunayoshiriki" alisema Kawemba.
Monday, June 13, 2016
Home »
» SHOMARI KAPOMBE KINARA TUZO ZA MCHEZAJI BORA AZAM FC
SHOMARI KAPOMBE KINARA TUZO ZA MCHEZAJI BORA AZAM FC
Related Posts:
MASHARTI LIGI KUU VODACOM DURU LA PILI Duru la Pili la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuanza kesho Jumamosi Desemba 17 kwa michezo minne kabla ya michezo mingine minne kufanyika siku ya Jumapili Desemba 18, mwaka huu. Katika mechi za kesho, Mabi… Read More
VIKOSI SIMBA, YANGA BAADA YA USAJILI DIRISHA DOGO Dirisha Dogo la Usajili limefungwa rasmi jana Alhamisi Disemba 15 majira ya Saa 6:00 usiku. Soka24 imefanikiwa kuvinasa vikosi vya miamba ya soka Tanzania Bara, Yanga na Simba baada ya kufungwa kwa dirisha hilo la usajili h… Read More
HIKI HAPA KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA MAAFANDE WA JKT Ligi kuu Tanzania Bara Mzunguko wa Pili. JKT Ruvu VS Yanga Siku: Jumamosi, Disemba 17, 2016 Muda: Saa 10:00 Jioni Kikosi Cha Yanga Leo. 1. Deogratius Munishi2. Juma Abdul3. Mwinyi Haji4. Kelvin Yondani5. Vic… Read More
Lionel Messi akaribia kuvunja rekodi ya Cristiano Ronaldo makundi ulaya Msimu huu huenda Lionel Messi akavunja au akaikuta rekodi iliyowekwa na Cristiano Ronaldo msimu wa 2015/16 wa kufunga jumla ya magoli 11 katika hatua ya makundi. Messi ambae ana magoli 92 na kilabu bingwa ulaya matatu … Read More
barcelona vs Real madrid ni EL CLASICO ya kihistoria Ubishi kumalizwa Camp Nou siku ya jumamosi wakati miamba miwili ya soka Barcelona na Real Madrid watakapoonyesha kazi katika mchezo muhimu wa ligi kuu ya nchini Hispania maarufu kama ‘LaLiga Santander’ Tukiiangalia … Read More
0 comments:
Post a Comment