Sunday, June 5, 2016

SAMATTA AIPA YANGA MBINU ZA KUIMALIZA TP MAZEMBE

Mchezaji wa zamani wa klabu ya TP Mazembe ya Congo, Mbwana Ally Samatta amesema Inawezekana Yanga kuifunga TP Mazembe


Samatta anayecheza katika klabu ya Genk ya nchini Ubelgiji ameonyesha kufurahishwa kwake baada ya timu ya Yanga kutinga hatua ya makundi kombe la shirikisho Afrika na amesema inawezekana kabisa kwa Yanga kuifunga timu yake ya zamani TP Mazembe.

Samatta amesema kikubwa ni Yanga kujipanga vizuri kabla hawajakutana na vigogo hao wa soka Afrika na kuhakikisha wanapambana kikamilifu pale watakapokutana.

"Inawezekana kabisa Yanga kuifunga Mazembe lakini kama watajipanga vizuri kwa sababu mpira unabadilika na chochote kinaweza kutokea ilimradi wacheze kwa malengo" alisema Mbwana Samatta.

Akielezea kitendo cha Yanga kufika hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika, amesema hatua hiyo ni nzuri kwa maendeleo ya soka la Tanzania na itasaidia kutangaza mpira wa Tanzania na kuleta hamasa kubwa kwa wachezaji wa ndani kujituma zaidi.

Yanga imepangwa kundi moja na TP Mazembe, Medeama na MO Bejaia, na itacheza na TP Mazembe kati ya Juni 28 na 29.

Related Posts:

  • HUYU MWINGINE ALIYENASWA NA WEKUNDU WA MSIMBAZI Simba imemsainisha beki wa Mwadui Emmanuel Semwanza. Semwanza ameichezea Mwadui kwenye mzunguko wa pili baada ya kununuliwa kwenye kipindi cha usajili wa dirisha dogo akitokea African Lyon, tayari Beki huyo amesaini mkata… Read More
  • USAJILI SIMBA NI TISHIOMwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Pope ametamba kuwa wamejipanga kufanya usajili wa kisayansi zaidi lengo likiwa ni kupata kikosi imara kitakachowapa ubingwa msimu ujao. Kwa miaka mitatu mful… Read More
  • JUMA ABDUL, SALUM TELELA KUWAKOSA WAALGERIAWachezaji Juma Abdul na Salum Telela wataikosa mechi kati ya Yanga na Mo Bejaia, mechi ya kwanza katika hatua ya makundi kombe la shirikisho CAF. Telela na Juma Abdul hawatakuwepo katika kikosi kitakachoenda nchini Uturuki… Read More
  • KIPA YANGA ASAKA KLABU YA KUHAMIABaada ya Yanga kufanikiwa kumsajili mlinda mlango kutoka timu ya Tanzania Prisons, Ben Kakolanya, Mlinda mlango wa siku nyingi wa klabu hiyo, Benedictor Tinoco amesema ni wakati wake kuangalia sehemu gani atacheza msimu ujao.… Read More
  • MBUYU TWITE NDANI ISSOUFOU BOUBACAR NJE YANGA Habari njema kwa mashabiki wa Yanga ni kwamba Kiungo wao wa kimataifa wa Rwanda Mbuyu Twite ameongeza mkataba katika klabu hiyo. Ikiwa tayari Yanga imefanikiwa kuwasajili wachezaji wawili golikipa Beno Kakolanya kutoka Ta… Read More

0 comments:

Post a Comment