Thursday, June 9, 2016

PLUIJM AWACHIMBA MKWARA WACHEZAJI YANGA

Wachezaji wa Yanga walipewa mapumziko baada ya fainali ya kombe la shirikisho TFF, Kocha Pluijm ametoa onyo kwa wachezaji wote ambao watachelewa kufika kikosi hapo.


Yanga wameanza mazoezi ya kujiandaa na mchezo wao wa kwanza hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC). Kocha mkuu wa klabu hiyo Hans Van Pluijm amesema hatawavumilia wachezaji wote ambao watachelewa kuripoti mapema kambini kujiandaa na michuano hiyo.

"Tunaanzia ugenini na timu ambayo hatuijui sana, hivyo ni lazima kufanya maadalizi ya kutosha ili tukaweze kupambana, hatutaki kwenda kuwa wasindikizaji bali kutafuta taji ambalo ndiyo jambo la msingi kwetu" alisema Pluijm.

Pluijm aliongeza kuwa haoni sababu yoyote ya mchezaji kuchelewa kujiunga na kikosi chake na kwamba atakuwa mkali sana kwa wachezaji ambao watachelewa kuripoti bila kuwa na sababu za msingi.

Yanga inakibarua kizito cha kuhakikisha wanafuzu hatua hii ya makundi na kutinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo. Yanga ipo kundi moja na TP Mazembe ya DRC, MO Bejaia ya Algeria na Medeama ya Ghana na itacheza mchezo wake wa kwanza na MO Bejaia wiki moja ijayo huko nchini Algeria.

Related Posts:

  • TFF YAJA JUU SUALA LA KESSYShirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limesema litaingilia kati suala la mchezaji Ramadhan Kessy aliyesajiliwa na Yanga huku Simba wakikataa kuiandikia barua Yanga kumruhusu mchezaji huyo kuanza kuitumikia klabu hiyo. … Read More
  • SERENGETI BOYS KUIKALISHA SHELISHELI TAIFA WIKIENDI HIITimu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 "Serengeti Boys" watashuka dimbani jumapili hii kucheza na Shelisheli. Mchezo huo utapigwa uwanja wa taifa jijini Dar Es Salaam jumapili Juni 26, 2016. Kocha wa timu hiyo, … Read More
  • KIMESHAELEWEKA YANGA WAPYA WOTE RUKSA ISIPOKUWA HUYUWachezaji wote wapya wa Yanga wamethibitishwa kuwa huru kuanza kuitumikia klabu hiyo isipokuwa Hassan Ramadhan Kessy. Yanga imewasajili wachezaji watano hadi sasa ambao ni Andrew Vicent, Juma Mahadhi, Ben Kakolanya, Hassan… Read More
  • SIMBA WAZIDI KUWEKA NGUMU KWA YANGA KUHUSU KESSYKlabu ya Simba imesema kama si Yanga kuwapatia fedha hawataandika barua itakayomuidhinisha Hassan Ramadhan Kessy kucheza michuano ya Kombe la shirikisho CAF CC Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Simba, Za… Read More
  • KUMBE HIKI NDO KINACHOITAFUNA SIMBAKumekuwa na madai kwamba kuna kiongozi mmoja ndani ya klabu ya Simba kuwa anaihujumu klabu hiyo katika ligi kuu Vodacom. Rais Wa Simba Evans Aveva Uongozi wa klabu ya Simba umeamua kulivalia njuga suala hilo ili kubaina n… Read More

0 comments:

Post a Comment