Friday, May 13, 2016

TWITE NA BOSSOU WAANZA RASMI MAZOEZI


Yanga wapo katika maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo wao wa hatua ya mtoano kombe la shirikisho barani Africa dhidi ya Sagrada Esperanca ya Nchini Angola, wakati kikosi cha Yanga kikijiweka fiti kuukabili mchezo huo, nyota wake wawili Vicent Bossou na Mbuyu Twite Jr wakianza mazoezi rasmi baada ya majeraha waliyoyapata katika mchezo wao dhidi ya Mbeya City
Bossou na Twite wameanza mazoezi leo Uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini, Dar es Salaam.
Twite aliumia goti wakati Bossou alipigwa kiwiko.

0 comments:

Post a Comment