Friday, May 27, 2016

NADIR HAROUB AMTOLEA NJE MAZIMA MKWASA KUJIUNGA NA TIMU YA TAIFA

Mchezaji Mkongwe wa timu ya Yanga na Taifa, Nadir Haroub maarufu kama Cannavaro, amekataa kabisa kujiunga na timu ya Taifa itakayocheza dhidi ya Kenya katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki.



Cannavaro amesema hawezi kuitikia wito huo kwa kuwa tayari yeye alishaandika barua ya kuacha kuitumikia timu ya Taifa na kuelekeza nguvu zake katika klabu yake ya Yanga.

"Naheshimu uteuzi wa Kocha Mkwasa na pia nafurahi kuona jina langu miongoni mwa majina 26 ya wachezaji walioitwa kwenye kikosi cha Stars, lakini haitakuwa rahisi kwangu kurudi kuichezea timu hiyo kwasababu nilishatangaza kustaafu na barua niliiandikia shirikisho (TFF),naomba kocha anisamehe kwa hilo" alisema Cannavaro.

Nadir alitangaza kuacha kuitumikia timu ya taifa baada ya Mkwasa kumvua unahodha wa timu hiyo na kumpa Mbwana Samatta bila kumjulisha kabla ya uamuzi wake huo, kitendo ambacho Cannavaro hakukifurahia.

Related Posts:

  • YANGA YAENDELEA KUJIWEKA FITI KLABU ya Dar Young Africans imeendelea na mazoezi huko mwanza katika viwanja vya DIT wakijiandaa na mchezo wao dhidi ya Toto Africans ambao utachezwa siku ya Jumamosi April 30, Yanga ambayo inashika nafasi ya kwanza kw… Read More
  • SIMBA WAREJEA DAR TAYARI KWA KUIVAA AZAM FC TIMU ya Simba Sports Club imewasili jijini Dar wakitokea visiwani Zanzibar ambako walikwenda kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Azam FC. Simba inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi inahitaji ushindi katika mchez… Read More
  • YANGA YAZIDI KUCHANJA MBUGA KAZI IMEBAKI KWA AZAM NA SIMBA LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea tena hivi leo katika viwanja 4, huko Jijini Mwanza wenyeji Toto Africans Wakiikaribisha Yanga. Mchezo huo ulioshuhudiwa na maelfu ya watazamaji ulikuwa na wa kuvutia ukizingatia kwamba t… Read More
  • TCHETCHE YUKO FITI KUIVAA SIMBA MSHAMBULIAJI hatari wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Kipre Tchetche, yupo fiti asilimia 100 kuivaa Simba  kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) utakaofanyika Uwanja wa Taifa, D… Read More
  • KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA TOTO AFRICANS KIKOSI CHA YANGA LEO. 1. Deogratius Munishi Dida. 2. Juma Abdul Japhary. 3. Oscar Fanuel Joshua. 4. Kelvin Patrick Yondani. 5. Vicent Bossou. 6. Salum Abo Telela. 7. Saimon Happygod Msuva. 8. Haruna Fadhil Niyo… Read More

0 comments:

Post a Comment