Friday, April 29, 2016

SIMBA WAREJEA DAR TAYARI KWA KUIVAA AZAM FC


TIMU ya Simba Sports Club imewasili jijini Dar wakitokea visiwani Zanzibar ambako walikwenda kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Azam FC. Simba inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kujiweka katika nafasi mzuri zaidi ya kushindania taji hilo la ligi msimu huu. Siku za hivi karibuni kumekuwa na kutokuelewana kwa baadhi ya wachezaji wa Klabu hiyo na kocha Mayanja kwa kile kinachoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu wa wachezaji hao. Simba inahitaji kutulia na kuweka tofauti zao pembeni kwa kipindi hiki ambacho ligi inaelekea ukingoni ili kuleta hamasa klabuni hapo na hatimaye kuchukua ubingwa wa ligi kuu. Mashabiki ambao walionekana kukerwa sana na matokea dhidi ya Coastal ambapo Simba walifungwa goli moja kwa bila wanatakiwa kuwa na subra na uvumilivu katika kipindi hiki na kuipa support timu yao ili ifanye vizuri.
Kwa upande mungine Kiungo mkabaji wa kimataifa wa klabu hiyo Justice Majabvi ambae alikuwa majeruhi nae alishiriki mazoezi ya timu wakiwa huko visiwani Zanzibar chini ya uangalizi wa Daktari wa timu Yassin Gembe na huenda kocha Mayanja akamtumia katika mechi yao dhidi ya Azam FC itakayochezwa siku ya Jumapili hii.

Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • NYOTA WATATU YANGA KUKOSA MCHEZO DHIDI YA MEDEAMA Klabu ya Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana lakini huenda wachezaji wake watatu wakaukosa mchezo huo kutokana na sababu … Read More
  • SHIZA KICHUYA ATUA MSIMBAZI Klabu ya Mtibwa Sugar imethibitisha kukamilisha uhamisho wa mchezaji wao Shiza Kichuya kujiunga na klabu ya Simba. Kwa muda mrefu kichuya alikuwa akihusishwa na kujiunga na wekundu hao wa Msimbazi lakini taarifa za hivi p… Read More
  • PICHA: SIMBA WALIVYOAGWA TAYARI KWENDA KUJIANDAA NA MSIMU UJAO Uongozi wa klabu ya Simba pamoja na wanachama na mashabiki wamekiaga kikosi cha Simba tayari kwenda kuanza mazoezi katika kambi itakayowekwa mkoani Morogoro kujiandaa na kuanza kwa msimu mpya wa ligi Kuu. … Read More
  • JERRY MURO: "TFF IMETANGA VITA NA YANGA" Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro amepinga vikali maamuzi ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF, kwa kudai kuwa haitambui adhabu hiyo na kwamba yeye ataendelea kufanya kazi. TFF imetoa adhabu ya kumfungia Jerry Mur… Read More
  • CANNAVARO AIPANIA MEDEAMA Nahodha wa timu ya Yanga, Nadir Haroub "Cannavaro" amesema Ushindi kwenye mechi dhidi ya Medeama ni lazima. Yanga inashiriki michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC) hatua ya makundi na tayari imeshacheza me… Read More

0 comments:

Post a Comment