Thursday, April 28, 2016

Arsenal Wakiwapata Wachezaji Hawa 3 Wa Seria A, Watamaliza Tatizo La Ushambuliaji


Arsenal wanahitaji kuboresh kikosi chao katika eneo lao la ushambuliaji, ambalo linaonekana kutokuwa imara kulikochangiwa pia na kuondoka kwa Mshambuliaji Robin Van Persie aliekajiunga na mahasimu wao Man United.
Ufungaji wa magoli katika kikosi hicho umekuwa si wa uhakika sana, safu hiyo ikiongozwa na Olivier Giroud na Danny Welbeck wanaofanya vizuri lakini si kwa kiwango kile cha Mholanzi Van Persie.
Kupata magoli hasa katika mechi za nyumbani limekuwa ni tatizo ambalo Arsenal wanapaswa kulifanyia kazi na bila shaka wanalijua hilo na watalifanyia kazi katika msimu ujao wa usajili.

Hapa nimekuwekea wachezaji watatu wanaocheza ligi kuu ya Italia Seria A ambao endapo watatua Arsenal basi  watakuwa wameimarisha safu yao ya ushambuliaji.

3. MAURO ICARD (INTER MILAN)
Huyu ni Muagentina mwenye miaka 23 ambae ubora wake katika eneo la ushambuliaji limemfanya atambulike katika ulimwengu wa soka duniani. Icard ni mchezaji wa zamani wa Barcelona katika kikosi cha vijana, alianza kwa kujiunga na Sampdoria na badae kujiunga na Inter amekuwa na mchango mkubwa sana klabuni hapo. Kwa sasa ni nahodha wa Inter Milan na anauwezo mkubwa unaomfanya awe forward mzuri kitu ambacho Arsenal wanakikosa kwa sasa.
Katika misimu mitatu amefunga jumla ya magoli 51 akiwa Inter katika mashindano yote na kiwango chake bado kinaonekana kukua zaidi, haitakuwa rahisi kumtoa Inter lakini kutua kwake Arsenal utakuwa ni uwekezaji mkubwa sana kwa klabu.
Ni mzuri katika umaliziaji na anaujuzi wa kumiliki mpira, na huwa anajua kuzitumia chance anazozipata katika kuwashangaza mabeki wa timu pinzani.
Mauro Icard

2. ALVARO MORATA (JUVENTUS)
Morata ni straika wa tofauti ukimlinganisha na Icard, mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid ni Straika mzuri sana katika kuunganisha timu, ni mchezaji ambae anauwezo wa kuwaweka wachezaji wenzake katika mchezo, na atakuwa na mchango mzuri sana Arsenal.
Giroud anafanana kiuchezaji na Morata lakini uwezo wa umaliziaji wa Morata ni mkubwa zaidi ukilinganisha na Giroud na utakuwa ni muunganiko mzuri sana akitua Arsenal akishirikiana na Mesut Ozil na Alex Sanchez.
Kwa sasa hana uhakika sana wa kuanza katika kikosi cha kwanza na hiyo inaweza kumfanya awe sokoni katika msimu ujao wa usajili.
Alvaro Morata
1.. GONZALO HIGUAIN (NAPOLI)
Higuan ni mchezaji mzuri aliyekatika level za juu katika rekodi za soka duniani, amefunga magoli 30 katika mechi 32 alizocheza msimu huu katika ligi ya Itali Seria A na endapo Arsenal wakiliona hilo na kumsajili atakuwa na mchango mkubwa sana katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo. Higuan huwa anatumia vizuri makosa ya mabeki wa wapinzani. Arsenal hawajawahi kuwa na straika wa kaliba ya Higuan kwa misimu ya hivi karibuni. Mchezaji ambaye amekamilika katika kila idara na endapo Mzee wenga ataamua kumwongeza katika kikosi chake ni wazi kuwa atakuwa ni chanzo cha magoli katika klabu ya Arsenal.

Gonzalo Higuan



Je, Unadhani moja kati ya Wachezaji hawa atasaidia kutatua matatizo ya safu ya Ushambuliaji Arsenal? Weka COMMENT yako katika sehemu ya comment hapo chini.



0 comments:

Post a Comment