Home »
Kitaifa
» MAMBO MATATU YANAYOMPA HOFU KOCHA PLUIJM ENDAPO MANJI ATAPIGWA CHINI YANGA
Yanga imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi hiki ambacho ipo chini ya uongozi wa Yusuf Manji, na Uchaguzi wa Yanga uko karibuni kufanyika. Tayari kocha wa timu hiyo Hans Van Pluijm ameonyesha wasiwasi wake kama ikitokea Manji akaachia madaraka au kupigwa chini klabuni hapo.
Gharama za timuRipoti zinasema kuwa timu ya Yanga inatumia zaidi ya Sh. Milioni 95 katika mechi 2 za kimataifa ambazo Yanga inacheza dhidi ya timu moja, fedha hizo zikiwa zinalipwa na Manji, hivyo kuondoka kwake kunampa Hans hofu kubwa.
Mishahara Minono Inayolipwa kwa Wachezaji Na Viongozi wa Benchi la Ufundi na Makocha.Hakuna ubishi kuwa kikosi cha Yanga kwa sasa ni miongoni mwa vikosi bora zaidi Afrika Mashariki na hii inatokana na kazi Nzuri ya Manji kwa kuwalipa vizuri wachezaji, viongozi wa Benchi la Ufundi pamoja na makocha kiujumla. Hivi juzi viongozi wa Simba walisikika wakisema kilichowafanya wachelewe kuwalipa wachezaji mishahara yao kwa wakati ni kuchelewa kwa fedha hizo kutoka kwa wadhamini wao, lakini kwa upande wa Yanga Manji anatoa pesa zake pale za wadhamini zinapochelewa ili tu kuweka hali ya utulivu klabuni hapo.Pia huduma nzuri ambazo Yanga inazipata chini ya Uongozi wa wake.
UsajiliTimu ya Yanga kwa sasa imejumuisha wachezaji mbalimbali kutoka katika sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi, Kocha Hans anamsajili mchezaji yoyote anayemtaka kutokana na ushirikiano mzuri anaoupata kutoka kwa bosi wake. Wachezaji wanaboreshewa mikataba yao kitu kinachowafanya wajitume na kuipenda kazi yao hali inayolenda matokeo chanya kwa wanajangwani.
Licha ya hofu zote hizo anazokumbana nazo Hans, uchaguzi wa Yanga ndo utakaoamua nani atashika hatamu katika klabu hiyo.
Related Posts:
Hiki Ndio Kikosi Cha Yanga Leo Dhidi Ya Mtibwa Sugar
LIGI KUU || TZ - BARA || 2015~2016.
YANGA SC Vs MTIBWA SUGAR FC.
UWANJA - Uwanja wa Taifa.
Muda - saa 10 : 00Alasiri.
>>>>>>KIKOSI CHA YANGA LEO<<<<<<<<
1. Deogratias Bonave… Read More
Misri Waihofia Stars AFCON
Timu ya taifa ya Misri katika kile kinachoonekana kupania kuiondoa Taifa Stars katika michuano ya kufuzu mashindano ya Afcon 2017, wapo nchini kuifuatilia Stars kila hatua.
Taarifa zinasema Meneja wa Timu hiyo yupo nchi… Read More
Simba Nayo Sasa Ni Ya Kimataifa
Simba SC ya jijini Dar es salaam imethibitisha kushiriki michuano ya Kombe la Nile Basin Club Championship, inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) itakayoanza kutumia vumbi Mei 22, 20… Read More
Kapombe Kutua Bongo
BEKI kisiki wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Shomari Kapombe, amerejea nchini jana jioni baada ya wataalamu wa Hospitali ya Morningside Mediclinic ya jijini Johannesburg, Afrika Kusini kurishidhwa na … Read More
Tambwe Amechuja Awekwe Benchi
Mashabiki wa Klabu ya Dar Young Africans wameonyesha kutokufurahishwa na kiwango kinachoonyeshwa na mshambuliaji wao Amis Tambwe siku za hivi karibuni.
Tambwe ambe ana magoli 18 katika orodha ya wafungaji bora msimu huu an… Read More
0 comments:
Post a Comment