Hali imekuwa sio ya kawaida kati ya Alex Sanchez na manager
wake Arsenal Wenger, Sanchez alitolewa katika mchezo dhidi ya Norwich zikiwa
zimebaki dakika sita mchezo kumalizika, kitendo hicho hakikumfurahisha Sanchez
na alivyotoka hakutaka hata kupeana
mkono na Wenger na akaenda moja kwa moja katika vyumba vya kubadilishia nguo,
ikionekana wazi kuwa alichukizwa na kitendo cha kutolewa katika mchezo huo.
Imeripotiwa
kuwa Sanchez ataihama klabu hiyo mara baada ya mkataba wake kumaliza hapo 2018.
Sanchez ameonekana kutokuwa na msimu mzuri kutokana na
kiwango chake kuonekana kimeshuka, lakini kocha Wenger amekanusha uvumi kwamba
hana maelewano mazuri na mchezaji huyo kufuatia kitendo alichokifanya Sanchez,
huku akisema kitendo cha Sanchez kuonyesha kuchukia baada ya kutolewa uwanjani
ni kuonyesha kwamba alikuwa anatamani aendelee kucheza na sio kwamba kuna
tofauti baina yao.
Lakini habari za ndani ya klabu hiyo zinaonyesha Wenger
hafurahishwi na kiwango na mchezaji huyo kwa sasa. Arsenal wanacheza na
Manchester City leo na licha ya hali inavyoendelea klabuni hapo baina ya Wenger
na Sanchez, mchezaji huyo anategemewa kucheza katika mechi hiyo.
0 comments:
Post a Comment