Sunday, May 8, 2016

HABARI 5 KUBWA ZA USAJILI ULAYA LEO MAY 8,2016


Rodgers Kurudi Swansea
Imeripotiwa kwamba Rodgers aliyekatimuliwa na Liverpool amekubali kurudi katika Klabu yake ya zamani ya Swansea kwa Mshahara wa Paundi 90,000/- sawa na zaidi ya Sh. Milioni 284 kwa wiki.

Szczesny Aishauri Chelsea Kuhusu Nainggolan
Mlinda mlango wa zamani wa Arsenal Szczesny anayecheza katika klabu ya Roma kwa sasa ameishauri Chelsea kumnunua Mbelgiji mwenzake Nainggolan, huku ikiripotiwa kuwa Szczesny ndio muunganishaji mkubwa wa hiyo dili.

Wenger Akiri Kumuhitaji Kante
Kocha Mfaransa Arsene Wenger anaamini midfielder wa Leicester City amekuwa ni miongoni mwa wachezaji walioonyesha kiwango cha hali ya juu zaidi katika ligi msimu huu, na anahakika kwamba licha ya wao kumuhitaji, vitajitokeza vilabu vingi kuonyesha nia ya kumnasa mchezaji huyo.

Sturridge Asema Hana Tatizo Na Klopp
Mshambuliaji wa klabu ya Liverpool Daniel Sturridge ametupilia mbali uvumi unaomuhusisha yeye na hatima yake katika klabu ya Liverpool, akisisitiza kwamba anafurahia maisha katika klabu hiyo huku akisema kwamba hakuna ufa kati yake na Klopp. Sturridge anahusishwa na kujiunga na klabu ya Arsenal, baada ya Wenger kuonyesha kutaka kuinasa saini ya mchezaji huyo.

Ben Arfa Katika Mazungumzo Na Barcelona

Nyota huyo mwenye miaka 29 amekuwa ni moja kati ya wachezaji walioonyesha kiwango bora zaidi katika Ligi kuu Ufaransa maarufu kama Ligue 1, huku Mkataba wake na klabu yake ukiwa unaisha mwishoni mwa msimu huu, Barcelona wameonyesha nia ya kutaka  kumsajili nyota huyo.

Related Posts:

  • KIUNGO MPYA SIMBA TISHIO KWA MKUDE, NDEMLASimba imefanikiwa kumsajili Kiungo Mzamiru Yasini akitokea katika klabu ya Mtibwa Sugar. Yasini amesema hayupo tayari kukaa benchi hivyo atahakikisha anapambana na wakongwe ili kujihakikishia nafasi yake katika kikosi cha … Read More
  • HUYU NDO KOCHA MPYA BRAZILTite ametajwa kuwa kocha mpya wa Brazil baada ya Dunga kutupiwa virago kufuatia matokeo mabovu waliyoyapata Brazil Copa America 2016. Tite Tite 55, anachukua nfasi ya Dunga aliyetimuliwa mara baada ya Brazil kutolewa hatu… Read More
  • KOCHA MWENYE REKODI ZA KIMATAIFA KUTUA SIMBAHarakati za usajili katika klabu ya Simba bado zinaendelea na habari za hivi karibuni zinasema makocha wanne kutoka katika nchi nne tofauti wamejitokeza kutaka kuinoa klabu hiyo. Geofrey Nyange "Kaburu" (Makamu mwenyekiti … Read More
  • CHIRWA ATUA JANGWANI KWA SH. MILIONI 240Mshambuliaji raia wa Zambia, Obrey Chirwa amejiunga na Yanga kwa dau la sh. Milioni 240 akitokea katika klabu ya FC Platinum za Zimbabwe. Chirwa ameifungia Platinum mabao matano katika mechi nane alizocheza kwenye ligi kuu… Read More
  • RUVU SHOOTING KUKIPA NGUVU KIKOSI CHAORuvu Shooting ipo katika mipango ya kusajili wachezaji saba ili kujiimarisha kabla hawajaanza kipute cha ligi kuu Vodacom msimu wa 2016/17. kwa sasa Ruvu Shooting inaendelea na kambi kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwa… Read More

0 comments:

Post a Comment