Rodgers Kurudi Swansea
Imeripotiwa kwamba Rodgers aliyekatimuliwa na Liverpool
amekubali kurudi katika Klabu yake ya zamani ya Swansea kwa Mshahara wa Paundi
90,000/- sawa na zaidi ya Sh. Milioni 284 kwa wiki.
Szczesny Aishauri Chelsea Kuhusu Nainggolan
Mlinda mlango wa zamani wa Arsenal Szczesny anayecheza
katika klabu ya Roma kwa sasa ameishauri Chelsea kumnunua Mbelgiji mwenzake
Nainggolan, huku ikiripotiwa kuwa Szczesny ndio muunganishaji mkubwa wa hiyo
dili.
Wenger Akiri Kumuhitaji Kante
Kocha Mfaransa Arsene Wenger anaamini midfielder wa Leicester
City amekuwa ni miongoni mwa wachezaji walioonyesha kiwango cha hali ya juu
zaidi katika ligi msimu huu, na anahakika kwamba licha ya wao kumuhitaji,
vitajitokeza vilabu vingi kuonyesha nia ya kumnasa mchezaji huyo.
Sturridge Asema Hana Tatizo Na Klopp
Mshambuliaji wa klabu ya Liverpool Daniel Sturridge
ametupilia mbali uvumi unaomuhusisha yeye na hatima yake katika klabu ya
Liverpool, akisisitiza kwamba anafurahia maisha katika klabu hiyo huku
akisema kwamba hakuna ufa kati yake na Klopp. Sturridge anahusishwa na kujiunga na klabu ya Arsenal, baada ya Wenger kuonyesha kutaka kuinasa saini ya mchezaji huyo.
Ben Arfa Katika Mazungumzo Na Barcelona
Nyota huyo mwenye miaka 29 amekuwa ni moja kati ya wachezaji
walioonyesha kiwango bora zaidi katika Ligi kuu Ufaransa maarufu kama Ligue 1,
huku Mkataba wake na klabu yake ukiwa unaisha mwishoni mwa msimu huu, Barcelona
wameonyesha nia ya kutaka kumsajili
nyota huyo.
0 comments:
Post a Comment