Sunday, May 15, 2016

JUVENTUS YAISHUSHIA KIPIGO KIKALI SAMPDORIA


Mabingwa wa ligi kuu nchini Italia Juventus, jana wametoa kipigo kikali kwa timu ya Sampdoria kwa kuichapa magoli 5 – 0, Juventus tayari walishakuwa mabingwa hata kabla ya mchezo wao dhidi ya Sampdoria na sasa wamefikisha jumla ya pointi 91 katika nafasi ya kwanza huku wakifuatiwa na Napoli katika nafasi ya pili waliojikusanyia pointi 82 kwenye michezo 38 waliyocheza.
Magoli ya Juve yalipachikwa nyavuni na Patrick Evra aliyefunga dakika ya 5, Paul Dybala akifunga magoli mawili dakika ya 15  na 37, magoli mengine yalifungwa na Chiellini dakika ya 77 na Bonucci akafunga karamu hiyo ya magoli alipofunga goli la 5 dakika ya 85.

0 comments:

Post a Comment