Monday, May 23, 2016
HUYU NDO ATAKAE AMUA FAINALI FA CUP KATI YA YANGA NA AZAM FC
Mwamuzi mahiri nchini, Israel Mujuni Nkongo wa Dar es Salaam, Jumatano Mei 25, 2016 ameteuliwa kuwa mwamuzi atakayechezesha mchezo wa fainali za Kombe la Shirikisho maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) itakayozikutanisha timu za Young Africans na Azam FC; zote za jijini Dar es Salaam.
Mchezo huo utakaoanza kesho saa 10.30 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam waamuzi wasaidizi watakuwa Ferdinand Chancha wa Mwanza (line 1) na upande wa pili ni Soud Lila wa Dar es Salaam (line 2) na mwamuzi wa akiba mezani ni Frank Komba wa Dar es Salaam pia. Kamishna wa mchezo huo anatakuwa Juma Mgunda wa Tanga.
Kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu msimu 2015/16, mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu 2015/16 wataiwakilisha nchi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2016/17. Nafasi hiyo imechukuliwa na Young Africans.
Kadhalika Azam ina tiketi tayari ya kushiriki Kombe la Shirikisho Barani Afrika kwa kufika fainali za ASFC ingawa kanuni zinataka bingwa ambako kwa upande wa Yanga wana tiketi ya michuano ya juu zaidi ya shirikisho. Mvuto wa mchezo wa Jumatano ni ushindani wa soka na zawadi kwa bingwa.
Fainali za Kombe la Shirikisho zinakuja baada ya mchuano ulioshindanisha timu 64 za Ligi Kuu Tanzania Bara - VPL (16); Ligi Daraja la Kwanza -FDL (24), Ligi Daraja la Pili – SDL (24).
Related Posts:
Kocha Mwadui Aitabiria Ubingwa Yanga Kocha wa klabu ya Mwadui FC, Ali Bushiri ameitabiria ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara (VPL 2016/17) klabu ya Yanga kufuatia kandanda safi liliopigwa na vijana hao wa Jangawani wakati timu yake ya Mwadui FC ilipolala kwa jum… Read More
Kipa Kagera Sugar Afariki Dunia Mlinda mlango wa Kagera Suga, David Burhani Amefariki dunia katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza. Taarifa kutoka kwa viongozi wa Kagera Sugar zinasema marehemu alikuwa akisumbuliwa na Malaria. Taarifa zaidi zinae… Read More
Serengeti Boys hiyooo AFCON U17, 2017 Serengeti Boys … Read More
16 Bora Azam Federation Cup ratiba yatangazwa, michezo 8 kufanyika kwa siku tatu tofauti Michuano ya kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) hatua ya 16 bora kutimua vumbi February 24 na February 26 na march 7 katika mikoa sita ya Tanzania Bara. February 24 kutakuwa na michezo minne katika mikoa min… Read More
Mkwasa Arejea Yanga Charles Boniface Mkwasa ameteuliwa kuwa katibu mkuu Yanga Afrika kwa mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa katibu mkuu Baraka Deusdedit anarejea katika nafasi yake ya awali ya utunza fedha. Akizungumza baada ya kurejea kik… Read More
0 comments:
Post a Comment