Wednesday, April 13, 2016

Yanga Na Azam Fc Zasusia Ratiba Kombe La FA

Hili ndo Kombe La ASFC
Yanga na Azam Fc zimesusia Ratiba ya michuano ya Azam Sports Federation Cup hatua ya nusu fainali iliyopangwa kufanyika  April 24 mwaka huu. Timu zote zimetoa sababu ya kushiriki michuano ya kumataifa, Michuano ambayo imekaribiana na ratiba hiyo ya ASFC. Azam Fc imepangwa kukutana na Mwadui ambapo mechi ya kwanza itapigwa Mkoani Shinyanga huku Yanga ikisafiri kuifuata Coastal Union Jijini Tanga.

Kiongozi wa Azam Fc Kawemba alisema watacheza mechi Tunisia tarehe 20 kwa maana hiyo wataondoka huko tarehe 21, hivyo itakuwa vigumu kufika Tanzania na kusafiri tena kwenda Mwadui kucheza mechi hiyo ya nusu Fainali.
Aliongeza kwa kulishauri shirikisho la mpira Tanzania TFF kuangalia uwezekano wa kuisogeza mbele michuano hiyo ili kila timu ipate nafasi ya kujiandaa vizuri.

Fainali ya michuano hiyo ya Kombe la shirikisho inatarajiwa kufanyika wiki moja baada ya ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom kumalizika.

Related Posts:

  • YANGA WAMWONGEZEA MKATABA PLUIJM Mabingwa wa ligi kuu Vodacom na wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika (CAF CC), Yanga wamemwongezea mkatabawa miaka miwili kocha wao Hans Van Pluijm. Kocha huyo ambaye ame… Read More
  • SIMBA WAIPANIA NDANDA FC Katibu mkuu wa Simba, Patrick kahemela ameapa kurudisha furaha na kuachana na machungu ya kutoka vichwa chini katika mechi zao za ligi kuu. Kiongozi huyo amesema Ndanda FC ndiyo itakuwa ya mfano kwani imepania kuwapa raha… Read More
  • HII NDO SABABU YA YANGA KUTOKUUZA WACHEZAJI ULAYA Kocha mkuu wa Yanga, Hans van Pluijm amesema wachezaji wengi wa Tanzania hawako tayari kucheza mpira wa kulipwa ulaya. Kwa muda mrefu imeonekana kuwa Yanga inawabania sana wachezaji wake hasa pale wanapopata nafasi ya kut… Read More
  • NAMUNGO FC YAPIGWA FAINI, YAPANDA DARAJA Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeipiga faini ya Sh. 500,000, Klabu ya Namungo FC ya Lindi kwa kila mechi ambayo mchezaji Imani Vamwanga aliichezea timu hiyo akitumia jina la Emmanuel T.… Read More
  • MWASHIUYA KUIKOSA MEDEAMA SC GHANA Kiungo klabu ya Yanga, Geofry Mwashiuya ataukosa mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Medeama SC utakaopigwa nchini Ghana kutokana kuuguza majeraha ya goti. Mwashiuya amewekewa bandeji laini ambayo inamsaidia kupona hara… Read More

0 comments:

Post a Comment