Wednesday, April 13, 2016

Kiiza, Juuko Murshid Kikaangoni Msimbazi


Tayari Simba wameanza kuangushiana lawama za chinichini. Jambo ambalo si sahihi lakini wapo ambao walikuwa chanzo cha kuua umoja katika mechi hiyo au kutokuwa makini, kukachangia wao kung’oka.

Kiiza&Juuko kikaangoni:
Kocha Jackson Mayanja, alilazimika kuwaweka benchi beki Juuko Murshid na mshambuliaji Hamisi Kiiza kutokana na kuchelewa kwao kurejea kambini.
Mayanja aliamini hawakuwa fiti, akafanya hivyo, jambo ambalo kocha yeyote mwenye kuijua kazi yake angefanya hivyo.
Wachezaji hao wawili ambao wote ni tegemeo, wamechangia kwa kiasi kikubwa Simba kufungwa kwa kuwa kukaa kwao nje, kulichangia Simba kushindwa kufanya vema. Kiiza aliingizwa kipindi cha pili akafunga.
Huenda angekuwa fiti, angesaidia kuanzia kipindi cha kwanza. Wanapaswa kulaumiwa kwa kuwa walijua Simba ipo kambini kwenye maandalizi muhimu ya mechi ya mtoano, vipi walibaki Uganda?

Maneno ya wachezaji wengine:
Kweli Kiiza na Juuko ni tegemeo. Lakini wameonyesha si wanaofuata weledi na huenda wameanza kulewa sifa, sawa. Lakini vipi waliokuwepo uwanjani hasa waliopata nafasi wakashindwa kuisaidia timu?
Maana yake kama Simba inacheza bila Kiiza wala Juuko haiwezi kushinda? Lazima wachezaji wajipime na wanapopata nafasi wazitumie na kuisaidia timu yao. Wao pia ni sehemu ya chanzo.

Viongozi nao je, wanasemaje!
Viongozi waliona mapema Kiiza na Juuko walikuwa “wakiwazingua”. Ajabu walitumia muda mwingi kulalamika badala ya kuchukua hatua.

Inawezekana bora kukosa kuliko mtu kuleta mchezo kazini tena kwa wao wanaolipwa mishahara minono.

Hawakupaswa kuwa kimya muda mrefu badala yake walitakiwa kuwabana mapema akina Juuko na Kiiza na hata adhabu ingekuwa mapema zaidi, huenda ingesaidia.

Sasa Simba, imetolewa katika michuano hiyo lakini Simba hawana wa kumlaumu badala ya wao wenyewe kuvurugana.

0 comments:

Post a Comment