Sunday, April 10, 2016

Kipre Tchetche Azifukuzia Rekodi Za Mbwana Samatta Ufungaji Bora CAF

MSHAMBULIAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Kipre Tchetche, ameingia kwenye orodha ya wachezaji wanne wanaofukuzia ufungaji bora wa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwaka huu.

Tchetche ameingia kwenye orodha hiyo baada ya kufunga mabao matatu wakati Azam FC ikiichapa Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwenye mchezo wa pili wa raundi ya kwanza ya michuano hiyo walipoichapa 4-3 na kufuzu raundi ya pili kwa ushindi wa jumla wa 7-3.

Mabao hayo yalimfanya mshambuliaji huyo kutoka Ivory Coast kuandika rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga ‘hat-trick’ mwaka huu ndani ya michuano hiyo, ambayo kuanzia kesho itafungua dimba kwa mechi za raundi ya pili.

Mchezaji huyo bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu wa 2013/14 Azam FC ilipotwaa ubingwa wa ligi hiyo bila kufungwa mchezo wowote, amelingana kwa mabao na washambuliaji wengine wawili ndani ya michuano hiyo kila mmoja akiwa ametupia wavuni mabao matatu.

Wachezaji hao aliokabana nao koo ni Amr Barakat anayekipiga Misr El-Makasa ya Misri pamoja na straika kutoka Harare City ya Zimbabwe, Raphael Manuvire, ambaye ndiye pekee timu yake imetolewa kwenye raundi ya kwanza.

Nyota hao wenye mabao matatu kwa pamoja wanamfukuzia straika Arsénio Sebastião Cabúngula ‘Love’, anayekipiga katika timu ya Sagrada Esperança kutoka nchini Angola, ambaye ndiye kinara wa mabao akiwa ameshatupia mabao manne mpaka sasa.

Tchetche ana nafasi ya kuwakimbiza na kuwapa presha wapinzani wake hao kwenye mbio hizo za ufungaji bora kama ataendeleza kasi yake ya upachikaji mabao kwa kutupia mabao, wakati Azam FC itakapoikaribisha Esperance ya Tunisia keshokutwa Aprili 10 katika mchezo wa raundi ya pili ya michuano hiyo na pia ule wa marudiano utakaopigwa Aprili 20 jijini Tunis.

Chanzo: Azamfc Official Site

Related Posts:

  • RASMI: PAUL NONGA AONDOKA YANGA Aliyekuwa mchezaji wa Yanga Paul Nonga ameondoka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Mwadui baada ya muda mrefu kuuomba uongozi wa klabu hiyo imuuze kwenye klabu ambayo atapata nafasi ya kucheza. Paul Nonga akisaini mkata… Read More
  • SIMBA WAIPANIA NDANDA FC Katibu mkuu wa Simba, Patrick kahemela ameapa kurudisha furaha na kuachana na machungu ya kutoka vichwa chini katika mechi zao za ligi kuu. Kiongozi huyo amesema Ndanda FC ndiyo itakuwa ya mfano kwani imepania kuwapa raha… Read More
  • KAULI ZA WACHEZAJI YANGA KUELEKEA MECHI DHIDI YA MEDEAMA Mabingwa wa Ligi kuu Vodacom na Wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika klabu ya Yanga inatarajiwa kushuka dimbani kesho kumenyana na Medeama SC kutoka nchini Ghana mchezo wa tatu hat… Read More
  • HII NDO SABABU YA YANGA KUTOKUUZA WACHEZAJI ULAYA Kocha mkuu wa Yanga, Hans van Pluijm amesema wachezaji wengi wa Tanzania hawako tayari kucheza mpira wa kulipwa ulaya. Kwa muda mrefu imeonekana kuwa Yanga inawabania sana wachezaji wake hasa pale wanapopata nafasi ya kut… Read More
  • JOSEPH OMOG AMPA USHAURI WA BURE PLUIJM Kocha mkuu mpya wa klabu ya Simba, Joseph Omog ametoa ushauri kwa klabu ya Yanga akiwaambia kuwa kama wanataka kufanya vizuri kwenye michuano ya shirikisho Afrika ni lazima wahakikishe wanazitumia nafasi za magoli wanazozipa… Read More

0 comments:

Post a Comment