Wednesday, March 16, 2016

MURO ASEMA HUU NI WAKATI WA UZALENDO

Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga watakuwa kibaruani Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuwavaa Al Ahly kutoka Misri katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.



Tayari wachuuzi, wameanza kuuza jezi za Al Ahly katika anga mbalimbali za jiji la Dar es Salaam.



Lakini hilo halijamtisha Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Yanga, Jerry Muro ambaye ameamua kuwaalika Simba na Azam FC waungane Jumamosi.
Muro amesema anaamini huu ni wakati wa uzalendo, wakati wa Utanzania na si upinzani wa Ligi Kuu Bara.

“Kweli nataka waje tuungane, kwani umesikia hata Simba nikiwatania? Sifanyi hivyo kwa kuwa ni kipindi cha kuungana.

“Hata Azam FC waje Jumamosi, mimi pia niende kuwashangilia Jumapili. Mambo ya utani yatarudi baada ya hii michuano ya kimataifa.



“Mfano Simba nao wakifuzu siku moja, nitaungana nao kuwashangilia. Sidhani kama ni sahihi kuwashangilia wageni wakati sisi ni Watanzania,” alisema Muro.

Related Posts:

  • YANGA YAWASILI SALAMA JIJINI MBEYA Timu ya Yanga imewasili salama jijini Mbeya Asubuhi ya leo wakitokea Dar, Kesho saa 10 : 00 alasiri mabingwa hao watashuka katika uwanja wa Sokoine kuwakabili wagonga nyundo Mbeya City! Jioni ya leo na kesho asubuhi Yan… Read More
  • HASSAN RAMADHANI KESSY AMWAGA WINO YANGA Beki wa kulia wa Simba SC, Hassan Ramadhani Kessy (katikati) akitia dole gumba kwenye fomu za Mkataba wa Yanga, Kessy amesaini miaka miwili kuitumikia Yanga kuanzia mwezi ujao. Zoezi hilo lilifanyika juzi usiku mjini Dar… Read More
  • TAZAMA MASHABIKI WA SIMBA WALIVYOLIANZISHA MSIMBAZI Kufuatia matokeo mabaya yanayoikumba klabu ya Simba katika mechi zao za hivi karibuni, mashabiki na wanachama wa klabu hiyo wameshindwa kuvumilia na kuamua kujikusanya katika makao makuu ya klabu hiyo kwa kile wanachodai … Read More
  • YANGA BINGWA TENA 2015/16 MCHEZO Kati ya Simba SC na Mwadui FC umemalizika kwa Mwadui kuibuka na ushindi wa goli 1 - 0. Simba walikuwa wanahitaji kushinda katika mechi hii ili kuisubirisha Yanga kutangaza ubingwa mapema, lakini hilo limeshindikan… Read More
  • MECHI 2 KALI ZA KUZITAZAMA LEO LIGI KUU TANZANIA BARA SIMBA SC VS MWADUI FC Simba leo wanawakaribisha Mwadui FC katika mchezo wa 27 wa Ligi kuu Tanzania Bara, Simba wanaingia katika mechi hii wakiwa na rekodi mbaya katika mechi za hivi karibuni, kwanii hutakiwi kukosa ku… Read More

0 comments:

Post a Comment