Wednesday, March 16, 2016

MURO ASEMA HUU NI WAKATI WA UZALENDO

Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga watakuwa kibaruani Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuwavaa Al Ahly kutoka Misri katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.



Tayari wachuuzi, wameanza kuuza jezi za Al Ahly katika anga mbalimbali za jiji la Dar es Salaam.



Lakini hilo halijamtisha Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Yanga, Jerry Muro ambaye ameamua kuwaalika Simba na Azam FC waungane Jumamosi.
Muro amesema anaamini huu ni wakati wa uzalendo, wakati wa Utanzania na si upinzani wa Ligi Kuu Bara.

“Kweli nataka waje tuungane, kwani umesikia hata Simba nikiwatania? Sifanyi hivyo kwa kuwa ni kipindi cha kuungana.

“Hata Azam FC waje Jumamosi, mimi pia niende kuwashangilia Jumapili. Mambo ya utani yatarudi baada ya hii michuano ya kimataifa.



“Mfano Simba nao wakifuzu siku moja, nitaungana nao kuwashangilia. Sidhani kama ni sahihi kuwashangilia wageni wakati sisi ni Watanzania,” alisema Muro.

Related Posts:

  • WAHISPANIA WAMWAGA WINO AZAM FC Uongozi wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, tayari umefikia makubaliano na wakufunzi kutoka  nchini Hispania, Kocha Mkuu Zeben Hernandez na Mtaalamu wa Viungo, Jonas Garcia. Makocha hao wawili wa… Read More
  • HIZI NDO SABABU ZILIZOPELEKEA AZAM FC KUPOKWA POINTI 3 Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limepitia marejeo ya uamuzi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) kuipoka pointi zake ilizovuna kutoka mchezo Na. 156 dhidi ya Mbeya City ya Mbeya katka mchezo uliofanyika Uwanja wa soko… Read More
  • SERENGETI BOYS YATINGA NUSU FAINALI Timu ya soka ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ leo Mei 19, 2016 imetinga hatua ya Nusu Fainali baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Korea Kusini  Timu ya soka ya Taifa ya Vijana wen… Read More
  • SHABIKI MKUBWA WA YANGA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI Shabiki Mkubwa Wa Yanga Askari Wa Jeshi La Polisi Kikosi Cha Usalama Barabarani Kinyogori Ameuawa Kwa kupigwa Risasi. Kinyogoli Enzi Za Uhai Wake Askari wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajini Kinyogor… Read More
  • YANGA; "KOMBE LA UBINGWA LIGI KUU HALINA HADHI" Ofisa habari wa klabu ya Yanga Jerry Muro amelikosoa kombe la ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara kwa kusema halina Hadhi. Akizungumza na waandishi wa Habari jana Muro alisema kombe hilo halina hadhi ukilinganisha na uku… Read More

0 comments:

Post a Comment