Friday, June 2, 2017

FA Yailipa Chelsea Paundi Milioni 150.8

Chama cha soka nchini Uingereza FA, kimeilipa klabu ya Chelsea kitita cha paundi milioni 150.8 ikiwa ni baada ya kushinda ubingwa ligi kuu nchini humo kwa msimu wa 2016/17.


Kutokana na mkataba wa matangazo ya televisheni, msimu wa 2016-17 kumeshuhudiwa ongezeko kubwa la fedha ukitoa takriban Paundi bilioni 2.4 kwa timu 20 zaidi ya msimu uliopita zilipolipwa Paundi bilioni 1.6.

Klabu ya Sunderland nayo licha ya kushuka daraja imepata kitita cha paundi milioni 93.471, fedha hizo zikitokana na matangazo ya Televisheni, mikataba ya kibiashara pamoja na zawadi.

0 comments:

Post a Comment