Timu ya Real Madrid
jana jioni iliendelea kujihakikishia nafasi ya kutwaa kombe la ligi kuu ya
Hispania ‘Spain - LaLiga Santander’ baada ya kuichapa timu ngumu ya Athletic
Bilbao 2 – 1 katika mchezo uliopigwa katika dimba la Athletic Bilbao uitwao San
Mames Barria.
Mchezo huo ambao
ulikuwa wa vuta nikuvute, uliwachukua Madrid dakika 25 kujipatia goli la
kuongoza baada ya Karim Benzema kumalizia kazi ya mchezaji bora duniani Cristiano
Ronaldo.
Athletic Bilbao wakicheza
kwa kujiamini na kuuutawala zaidi mchezo karibu muda wote na kusababisha
wachezaji wane wa Real Madrid kufanya madhambi na kuadhibiwa kwa kadi za njano
kwa dakika tofauti dakika ya 28 Daniel Carvajal(RM) na Aritz Aduriz(AB)
walivimbishiana kifua na refa kuwaadhibu wote kwa kadi za njano.
31’ Casemiro nae
alipewa kadi ya njano kwa mchezo mbaya, Toni Kroos na Keylor Navas dakika za 71
na 90 pia walionywa kwa kadi za njano.
Mpaka mapumziko Real Madrid
walikuwa na goli moja wenyeji wakiwa 0.
Kipindi cha pili
dakika ya 65 Raul Garcia alifanya kazi kubwa na kumuachia mpira Aritz Aduriz
ambae na yeye aliitumia vizuri na kuandika goli kwa timu yake na kufanya ubao
wa matangazo usomeke 1 – 1.
Kona iliyopigwa na
Toni Kroosdakika ya 68 ilitua kwenye kichwa cha Cristiano Ronaldo ambae
aliuparaza mpira huo na kumkuta Casemiro ambae aliukwamisha mpira huo wavuni na
kuipatia Madrid goli la pili na la ushindi.
Kwa ushindi huo Madrid
wamefikisha pointi 65 katika michezo 27 huku Barcelona wao wakiwa na pointi 60
kwa michezo 27.
Matokeo ya michezo
mingine ya jana march 18 ni kama ifuatavyo.
Real Betis 2 - 0
Osasuna
Eibar 1 - 1 Espanyol
Alaves 1 - 0 Real
Sociedad
Michezo mitano kupigwa
leo jumapili
Leganes VS Malaga 14:00
Atletico Madrid VS
Sevilla 18:15
Sporting Gijon VS
Granada 20:30
Deportivo La Coruna VS
Celta Vigo 20:30
Barcelona VS Valencia 22:45
Msimamo
wa Spain - LaLiga Santander baada ya jana march 18

0 comments:
Post a Comment