Wednesday, November 9, 2016

Azamu yamuenzi Mzee Said Mohamed Abeid kwa ushindi, Simba yaangukia pua Mbeya


Huko Mbeya wakicheza kwa tahadhari kubwa huku wakikumbuka vipigo viwili mfululizo walivyopata katika mechi zilizopita, timu ya Tanzania Prisons imeadhibu simba goli 2 – 1 katika mechi ya kukamilisha raundi ya kwanza.
Mchezo ulianza kwa simba kuliandama lango la wenyeji wao huku tukimshudia Mavugo, na Mnyate wakipoteza nafasi za wazi ambazo zingeipatia simba uongozi mapema, iliwachukua simba dakika 43 kujipatia goli kupitia kwa Mnyate baada ya kuunganisha kwa kichwa pasi safi ya Kichuya.
Kipindi cha pili Tanzania Prisons waligeuza aina ya mchezo na kuwazua simba kupiga krosi huku wakishambulia kwa kushtukiza na mnamo dakika ya 47’ na 64’ kupitia kwa Hangayaa .
Hadi mwisho wa mchezo huo Tanzania Prisons 2 simba 1.

Shinyanga mambo yamewaendea vizuri Azam Fc baada ya kupata ushindi wa kwanza mkubwa katika msimu huu baada ya kuitandika bila huruma timu ya Mwadui kwa magoli 4 – 1.
Mwadui ndio waliotangulia kuliona lango la Azam dakika ya 30 kupitia kwa Hassan Kabunda, mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika Mwadui 1 Azam 0.

Kipindi cha pili 54’ John Bocco aliisawazishia Azam, dakika ya 71 Shaaban Idd alifunga goli la pili dakika 74 Shaaban Idd alifunga la tatu na alifunga tena la nne na la tatu kwake.

Related Posts:

  • YANGA WAKABIDHIWA RASMI KOMBE LAO KLABU Ya Yanga imekabidhiwa kombe lao jioni ya leo katika uwanja wa taifa mara tu baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Ndanda FC, mchezo ambao umemalizika kwa sare ya 2 - 2. Ndanda FC ndio walikuwa wa kwanza kupata… Read More
  • NDANDA FC WAPANIA KUHARIBU SHEREHE YA YANGA Msemaji wa klabu ya Ndanda FC Idrisa Bandari amesema watahakikisha wanaifunga Yanga na kuharibu Sherehe yao ya kukabidhiwa kombe leo katika mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar. Yanga wanaingia katika mc… Read More
  • TFF YAZIKUMBUSHA TENA KLABU ZA LIGI KUU 2016/17 Kwa mara nyingine, Bodi ya Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka (TFF) imezikumbusha klabu zitakazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2016/17 kuwa mchakato wa wa utengenezaji kanuni umeanza tangu Mei 5, 2016. Bodi ya Ligi… Read More
  • AZAM FC YAICHAPA AFRICAN SPORTS Klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati Azam FC ilikuwa ugenini jijini Tanga kupambana na African Sports katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom. Azam FC wamefanikiwa kuibuka na ushindi katika mchezo h… Read More
  • SIMBA SC WAIDUNGUA MTIBWA SUGAR NYUMBANI KWAO SIMBA ilishuka dimbani hivi leo kucheza na Mtibwa Sugar katika mchezo wao wa 29 wa ligi kuu Tanzania bara,Mchezo uliopigwa mjini Morogoro. Mchezo huo umemalizika kwa Simba SC kushinda kwa goli 1 - 0 goli lililofungwa na… Read More

0 comments:

Post a Comment