Saturday, July 23, 2016

SUNDERLAND YAMRUDISHA DAVID MOYES UINGEREZA

Klabu ya Sunderland imemteua kocha wa zamani wa Manchester United David Moyes kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo baada ya Sam Allardyce kukabidhiwa kikosi cha timu ya taifa ya England.

Moyes anachukua mikoba ya Sam Allardyce katika dimba la Stadium Of Light. Moyes amesaini mkataba wa miaka minne na Paka hao Weusi na alionekana kuwa chaguo la mwenyekiti wa klabu hiyo Ellis kwa muda mrefu.

Moyes 53, aliyekatimuliwa na klabu ya Man United mara tu baada ya kukabidhiwa mikoba kufuatia kuondoka kwa kwa Alex Ferguson na kuwa na wakati mgumu na klabu hiyo bado yuko Hispania na klabu ya Real Sociedad kwa sasa na ataanza majukumu ya kuiongoza Sunderland msimu ujao.
Ungana Na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA  Kwa Habari Za Haraka Za Soka Kote Ulimwenguni.

0 comments:

Post a Comment