Sunday, July 24, 2016

BAADA YA KUTUPIWA VIRAGO HAMISI KIIZA AICHANA VIBAYA SIMBA

Hamisi Kiiza ambaye aliingia katika mgogoro na uongozi wa timu yake ya zamani ya Simba SC ameamua kufunguka na kusema kwamba timu hiyo hata isajili nyota wote kamwe haitafanikiwa.

Kiiza aliyeshika nafasi ya pili kwa upachikaji wa magoli ligi kuu Vodacom msimu wa 2015/16 akimaliza kwa kufunga jumla ya magoli 19 amesema Simba hata imsajili Mbwana Samatta anayetumikia klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji kamwe haitafika kokote mpaka pale baadhi ya viongozi waondoke katika klabu hiyo.

Mshambuliaji huyo amedai kwamba kitu kikubwa kinachowasumbua Simba ni uongozi na wala sio wachezaji na hata makocha ambao wamekuwa wakibadilishwa mara kwa mara.

“Sidhani kama kutakuwa na mabadiliko hata kama wakiwasajili wachezaji wote wanaofanya vizuri Tanzania, wamrudishe na Mbwana Samatta, tatizo kubwa lililopo Simba ni baadhi ya viongozi ambao wamekuwa na chuki na wachezaji hasa anaposema ukweli na kudai haki zake,” alisema Kiiza.

Kiiza aliongeza kuwa ameshindwa kumaliza mkataba wake na klabu hiyo kutokana na kutupiwa lawama nyingi katika klabu hiyo ikiwemo ile ya kuambiwa kuwa anaigawa timu, alisema kwamba ingekuwa kweli kuwa anaihujumu timu hiyo basi asingekuwa anafunga magoli pale alipokuwa anapata nafasi ya kufanya hivyo bali ni fitna tu za baadhi ya viongozi klabuni hapo ndio zinazoitafuna klabu hiyo huku akisisitiza kuwa Simba ilikuwa na nafasi ya kufanya vizuri msimu uliopita lakini tatizo kubwa ni huo uongozi.

Hata hivyo Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo Hanspoppe amekanusha tuhuma hizo na kusema kwamba ni benchi la ufundi kwa ujumla wake ndio halikuona haja ya kuendelea kuwa na mchezaji huyo (Kiiza) kutokana na utovu wa nidhamu.
Ungana Na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA 

Related Posts:

  • FARID MUSSA ATUA JIJINI DAR Farid Mussa Mchezaji Wa Timu Ya Azam FC Amewasili Jijini Dar Akitokea Hispania Alikokwenda Kufanya Majaribio Ya Kucheza Soka La Kulipwa Katika Klabu Ya Deportivo Tenerife Farid amewasili salama jijini Dar jana majira ya … Read More
  • HAYA NDO ALIYOAHIDIWA KOCHA PLUIJM YANGA Mkataba wa kocha mkuu wa Yanga Hans Pluijm ukiwa umebakiza siku chache kumalizika Yanga yafunguka juu ya kuendelea kubaki na kocha huyo. Klabu ya Yanga imeanza mazungumzo rasmi na kocha mkuu wa klabu hiyo Hans Van Pluijm… Read More
  • MBAO FC YAAHIDI MAKUBWA LIGI KUU Timu ya Mbao FC iliyopanda daraja Kufuatia maamuzi ya kamati ya Nidhamu ya TFF ya kuzishusha daraja timu 4 za kundi C na kuifanya Mbao kushika nafasi ya kwanza katika kundi hilo..Imeahidi kuwashangaza wapenda soka katika lig… Read More
  • SAKATA LA STAND UNITED KUWA KAMPUNI LAZIDI KULETA UTATA Wanachama na Mashabiki wa klabu ya Stand United Wamepinga suala ya timu yao kuendeshwa kama kampuni. Siku Chache zilizopita Soka24 ilikuletea taarifa juu ya kampuni ya ACACIA inayoidhamini klabu ya Stand United kutishia … Read More
  • DENIS KITAMBI KATIKA MTIHANI MZITO AZAM FC Kocha Msaidizi wa Azam FC  Denis Kitambi Ataiongoza klabu hiyo katika mchezo wa mwisho wa Ligi katika kuwania nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara. Ligi Kuu Tanzania Bara inaelekea ukingoni na mechi… Read More

0 comments:

Post a Comment