Friday, June 10, 2016

URUGUAY YATUPWA NJE YA MASHINDANO COPA AMERICA 2016

Timu ya taifa ya Uruguay imetolewa rasmi katika michuano ya Copa America inayoendelea huko nchini Marekani.


Uruguay inayaaga mashindano hayo baada ya kukubali kipigo cha goli moja kwa bila kutoka kwa Venezuela.

Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez alionekana kukerwa sana na hali hiyo hasa ukizingatia timu yake imefikia hatua ya kutolewa ikiwa yeye hajacheza mechi hata moja.

Akiwa benchi Suareza alionyesha wazi hasira zake kwa kupigapiga sehemu ambapo alikuwa amekaa. Kabla kipindi cha pili hakijaanza Suarez alionekana kupasha lakini hakupata nafasi ya kuingia uwanjani.

Kocha wa timu hiyo Oscar Tabarez alisema asingeweza kumchezesha Suarez kwa kuwa hakuwa fiti asilimia 100%.

"Mchezaji hayuko fiti kwa kucheza. Sitamchagua mchezaji ambaye hayuko fiti 100%. Alikasirika?, mimi hilo sijui. Kwangu mimi hajaniambia kitu chochote" alisema Tabarez.

Uruguay ambao ni mabingwa mara 15 wa michuano hii wa
metolewa katika hatua ya makundi kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1997.

Goli la ushindi la Venezuela lilipatikana dakika ya 36, baada ya kiungo Alejandro Guerra kupiga shuti lililopanguliwa na goli kipa na kugonga mwamba nae Solomon Rondon akaja kutupia nyavuni mpira huo.

Related Posts:

  • FIFA YAKATAZA WACHEZAJI KUSHEREHEKEA NA FAMILIA ZAO UWANJANIFifa inapanga kuzuia kitendo cha wachezaji kusherehekea ushindi na familia zao uwanjani katika michuano ya Euro inayoendelea huko nchini Ufaransa. Mkurugenzi wa mashindano hayo Martin Kallen amesema zuio hilo ni kutokana n… Read More
  • SHABIKI WA RONALDO APIGWA FAINIShabiki aliyevamia uwanjani na kumkumbatia Christiano Ronaldo wakati wa mechi ya robo fainali kati Ureno na Poland amepigwa faini ya paundi 500. Katika mechi ya robo fainali kati ya Ureno na Poland shabiki mmoja wa Ureno a… Read More
  • CHANGAMOTO SITA ANAZOKUMBANA NAZO GUARDIOLA MAN CITYKufuatial utambulisho wake kuwa kocha mkuu mpya wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola anatakiwa asilale aanze kazi mara moja akijaribu kutatua changamoto mbalimbali klabuni hapo. Ubora wa Guardiola umedhihirika akiwa … Read More
  • KOCHA WA ARGENTINA ABWAGA MANYANGA Gerardo Martino ameamua kuachana na kibarua cha kuifundisha timu ya taifa ya Argentina kufuatia matokeo mabaya Copa America 2016. Moja ya sababu zilizomfanya Martino kuachia nafasi hiyo ni ugumu wa kuwapata wachezaji wazu… Read More
  • MAN U WAANZA KUUZA JEZI NA. 9 YA IBRAHIMOVIC Kwa mujibu wa ripoti zilizoenea sana siku za hivi karibuni ni kwamba Zlatan Ibrahimovic anakaribia kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Man U. Tangu aondoke PSG kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu wa 2015/16, Zlatan… Read More

0 comments:

Post a Comment