Kocha Mkuu wa Yanga, Hans Van Pluijm ameliomba shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) kuchukua hatua kali kwa klabu ambazo mashabiki wake wataleta vurugu dhidi ya timu pinzani.
Pluijm ametoa onyo hilo kwa CAF wakati huu michuano ya kombe la shirikisho hatua ya makundi ikitarajiwa kuanza kutimua vumbi hivi karibuni, Yanga wakianza mchezo wao wa kwanza katika hatua hiyo dhidi ya MO Bejaia ya nchini Algeria, mechi itakayochezwa mwishoni mwa wiki hii.
Pluijm amesema kwa miaka mingi kumekuwa na vitendo vya vurugu kwenye mchezo wa soka barani Afrika hasa kwa timu mwenyeji kuifanyia vurugu timu ngeni.
Kocha huyo alitoa mfano wa vurugu ambazo Yanga walifanyiwa kwenye mchezo wa ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ugenini na dhidi ya Sagrada Esperanca ya nchini Angola.
"Vitendo vya vurugu dhidi ya timu ngeni katika soka Afrika sio vya sasa, vipo kwa miaka mingi sana. Sisemi natarajia kukutana navyo katika mchezo dhidi ya MO Bejaia au la, lakini tunatakiwa kujiandaa kisaikolojia kwa lolote" alisema Pluijm.
"CAF wanapaswa kuwa wakali dhidi ya vitendo hivi vya vurugu vinavyofanywa na timu wenyeji kwa wageni wao, wanatakiwa kuchukua hatua kali."
Yanga itacheza mchezo wa kwanza dhidi ya MO Bejaia Juni 19, kisha watarejea nchini kucheza TP Mazembe juni 28.
Bonyeza hapa ku-Like Page ya Soka24 Facebook
Wednesday, June 15, 2016
KOCHA YANGA ATOA ONYO KALI CAF
Related Posts:
MEDEAMA KUTUA DAR KESHO Wapinzani wa Yanga katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika, Medeama ya Ghana wanatarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa mchezo wa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga katika msimamo wa Kund… Read More
MSIMAMO KOMBE LA SHIRIKISHO BARANI AFRIKA CAF CC Msimamo Kombe La Shirikisho Barani Afrika 2016 (CAF CC) … Read More
NYOTA WATATU YANGA KUKOSA MCHEZO DHIDI YA MEDEAMA Klabu ya Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana lakini huenda wachezaji wake watatu wakaukosa mchezo huo kutokana na sababu … Read More
KAULI ZA WACHEZAJI YANGA KUELEKEA MECHI DHIDI YA MEDEAMA Mabingwa wa Ligi kuu Vodacom na Wawakilishi pekee Afrika Mashariki katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika klabu ya Yanga inatarajiwa kushuka dimbani kesho kumenyana na Medeama SC kutoka nchini Ghana mchezo wa tatu hat… Read More
HIKI NDO KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA MEDEAMA SC LEO KOMBE LA SHIRIKISHO BARANI AFRIKA (CAF CC) 2016HATUA YA MAKUNDIMCHEZO WA KUNDI A YANGA SC VS MEDEMA SC KIKOSI CHA YANGA LEO 1. Deogratius Bonaventura Munishi 2. Juma Abdul Mnyamani. 3. Oscar Fanuel Joshua. … Read More
0 comments:
Post a Comment