Saturday, May 14, 2016

SIR ALEX FERGUSON AKIRI KUFANYA KOSA KUBWA UNITED


Sir Alex Ferguson amekiri waziwazi kuwa maamuzi yake ya kutangaza kuwa angestaafu mwaka 2001 lilikuwa ni kosa kubwa katika maisha yake ya ukocha.

Kocha huyo wa zamani wa Man Utd Sir Alex Ferguson alikaa klabuni hapo kwa miaka 15 ndipo alipotangaza kuwa ataondoka klabuni hapo baada ya msimu mmoja mbele.
Lakini miezi 6 baadae Fergie aligundua kuwa alifanya kosa na akakubali kubaki Old Trafford.

“Kosa kubwa nililowahi kufanya nikiwa Manchester United ni kutangaza kuwa nitaachana na Man Utd mwanzo wa msimu” alisema Fergie akiiambia Daily Mirror.

“Nafikiri hicho kitu kiliwakatisha tama watu wengi, kujua Ooh! Kumbe kocha anaondoka, lakini nilipobadili maamuzi yangu mwezi January, nilianza kuifikiria tena United na ni kwa jinsi gani tungepambana kumaliza katika nafasi  za juu” aliongeza Ferguson.

Ferguson alikiri kuwa familia yake na viongozi wa timu walichangia katika kubadilisha maamuzi yake ya kustaafu ukocha na kuendele kubaki kuitumikia klabu hiyo.
alisema “Ni kitu kizuri kusikiliza ushauri wa viongozi na wafanyakazi wenzio”

“Mwaka 2005, kipindi hicho hatukufanikiwa kushinda taji lolote, wakati huo ambapo kabla nilitangaza kustaafu kuitumikia klabu na hicho kitu ndo kiliwaathiri wachezaji na watu wote”
“Lilikuwa ni kosa na mke wangu pamoja na watoto wangu 4 walisaidi kubadili mtazamo wangu, na nilianza kufikiri tena, baada ya hapo ndipo Wayne Rooney na Christiano Ronaldo wakajiunga na klabu na tukaanza kurudisha morali ya wachezaji na klabu”

Ferguson aliendelea kusema baada ya kujutia kosa lake hilo na kuamua kubaki katika klabu na mara baada ya Rooney na Ronaldo kuongeza nguvu katika kikosi cha United ndipo mambo yalibadilika na kuanza kushinda mataji ya ligi mara nyingi zaidi.

United inamaliza mechi zake za ligi jumapili hii katika uwanja wa Old Trafford dhidi ya Bournemouth, na baada ya hapo wataenda Wembley kucheza na Crystal Palace katika fainali ya FA Cup.

Related Posts:

  • JOHN BOCCO NJE AZAM DHIDI YA AFRICAN SPORTS NAHODHA wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’, ameingia kwenye orodha ya wachezaji majeruhi wa timu hiyo baada ya misuli yake ya mguu kukaza. Tokea jana mshambuliaji huyo amekuwa a… Read More
  • FAINALI UEFA CHAMPIONS LEAGUE KUAMUA HATIMA YA RONALDO MADRID Superstaa wa Real Madrid Christiano Ronaldo amekubali kubaki Real Madrid kwa Sharti moja tu. Ronaldo amesema yupo tayari kubaki Santiago Bernabeu ikiwa tu Real Madrid watafanikiwa kuifunga Atletico Madrid katika mchezo w… Read More
  • KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA NDANDA FC LIGI KUU TANZANIA BARA Ndanda SC Vs Young Africans SC  Uwanja : Taifa. Muda : Saa 10 : 00. Kikosi Cha Yanga. 1.Deogratius Munishi Dida. 2.Juma Abdul Jafary. 3.Mwinyi Haji Ngwali. 4.Vicent Bossou. 5.K… Read More
  • WACHEZAJI SIMBA WAGOMA KUCHEZA NA MAJIMAJI Hali ya sintofahamu imezidi kuimkumba klabu ya Simba, baada ya wachezaji wake 7 kususia mechi kati yao na Majimaji ya Songea itakayochezwa siku ya Jumatano May 11. Wachezaji hao sita ni wakigeni na mmoja ni wa ndani, wac… Read More
  • KIKOSI CHA SIMBA CHAPEWA LIKIZO FUPI SIMBA iliyotoka kucheza na Mtibwa Sugar jana na kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila goli lililofungwa na Abdi Banda, imepewa mapumziko mafupi kabla ya kuanza kujiandaa na mchezo wao wa mwisho wa ligi dhidi ya JKT Ru… Read More

0 comments:

Post a Comment