Mrisho Halfan Ngassa Mtanzania anayecheza katika klabu ya Free State ya Nchini Afrika Kusini amesema yupo tayari kurudi kucheza Yanga.
Winga huyo wa Kimataifa raia wa Tanzania anacheza katika klabu ya Free State inayoshiriki Ligi kuu nchini Afrika Kusini PSL. Alipozungumza na Goal Ngasa amesema yupo tayari kurudi Yanga ili kuongeza nguvu katika kikosi hicho hata kwa mkopo. "Nipo nchini kwa ajili ya mapumziko mafupi lakini nimekutana na viongozi Pamoja na kocha Hans Van der Pluijm, Wameonyesha nia ya kunihitaji katika hatua ya makundi na mimi nipo tayari kurejea nyumbani ila itakuwa vizuri kama wataongea na uongozi wa timu yangu Free State." alisema Mrisho Ngasa. Yanga ambayo ipo katika hatua za mwisho za maandalizi kabla hatua ya makundi kombe la shririkisho barani Afrika haijaanza kutimua vumbi, wanahitaji kuimarisha kikosi chao kwa kuwa na wachezaji wenye uzoefu mkubwa wa kucheza michuano ya kimataifa ili kuweza kuleta ushindani kwa wapinzani katika hatua hiyo.
VITA YA KUWANIA NAFASI YA PILI VPL KUENDELEA TENA LEO
LIGI kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo katika viwanja viwili. Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa watawakaribisha vijana wa Msimbazi Simba SC wakati huko Tanga Azam FC itachuana na African Sports.
Simba w…Read More
AMIS TAMBWE AMWOMBEA MABAYA KIIZA
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Dar Young Africans Amis Tambwe, amemaliza mchezo wa jana dhidi ya Ndanda FC bila ya kufunga goli, Tambwe anayeongoza katika orodha ya wafungaji bora katika ligi kuu Tanzania bara msim…Read More
MBEYA CITY, YANGA KUSIMAMISHA JIJI LEO
Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo utakaowakutanisha Mbeya City ya Jijini Mbeya dhidi ya Yanga ya jijini Dar-Es-Salaam. Yanga inaingia katika mchezo huu …Read More
VICENT BOSSOU AITWA TIMU YA TAIFA YA TOGO
Kocha mpya wa Togo Mfaransa Claude LeRoy amemuita Vicent Bossou katika kikosi cha timu yake ya Taifa .Bossou ameitwa kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha akiwa na klabu ya Yanga.
Tayari barua ya mualiko wa kujiu…Read More
NDANDA FC WAPANIA KUHARIBU SHEREHE YA YANGA
Msemaji wa klabu ya Ndanda FC Idrisa Bandari amesema watahakikisha wanaifunga Yanga na kuharibu Sherehe yao ya kukabidhiwa kombe leo katika mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar.
Yanga wanaingia katika mc…Read More
0 comments:
Post a Comment