Monday, May 30, 2016

JULIO NA NDOTO ZA UBINGWA WA LIGI KUU MSIMU UJAO

Kocha wa timu ya Mwadui FC, Jamhuri Kiwelu Julio anaamini ubingwa unawezekana katika msimu ujao wa ligi.





Julio amesema anajipanga vizuri kukiweka kikosi chake sawa ili waweze kutwaa ubingwa wa ligi msimu ujao. Kitendo cha Mwadui FC kumaliza katika nafasi ya 6 katika msimamo wa ligi kuu msimu wa 2015/16 kumemfanya Julio aamini kuwa timu yake inaweza kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu ujao.

Mwadui ambayo imeshiriki ligi kuu kwa mara ya kwanza msimu huu imeonyesha ushindani mkubwa katika ligi kwa timu zote ndogo na kubwa.

"Kama tumeweza kumaliza nafasi ya sita kwenye msimu wa kwanza basi hata ubingwa unawezekana kwa sababu ukiangalia tuliweza kucheza vizuri dhidi ya timu kubwa za Yanga, Azam na Simba na kufika nusu fainali ya Kombe la FA" alisema Julio akionyesha imani yake kubwa ya kutwaa ubingwa msimu ujao.

Julio aliongeza kuwa kikubwa  ni kufanya usajili wa uhakika wa wachezaji wenye uwezo mkubwa.

Related Posts:

  • SERENGETI BOYS KUIKALISHA SHELISHELI TAIFA WIKIENDI HIITimu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 "Serengeti Boys" watashuka dimbani jumapili hii kucheza na Shelisheli. Mchezo huo utapigwa uwanja wa taifa jijini Dar Es Salaam jumapili Juni 26, 2016. Kocha wa timu hiyo, … Read More
  • SUALA LA YANGA KUTAKA MECHI NA MAZEMBE ISOGEZWE MBELETFF imesema kuwa imepokea maombi ya Yanga ya kutaka shirikisho hilo kuiandikia CAF wakitaka mchezo wao wa Kombe la Shirikisho la Soka la Afrika(CAF-CC) dhidi ya TP Mazembe uchezwe Juni 29 badala ya Juni 28. “Yanga walipewa… Read More
  • NGASSA AUKUBALI MZIKI WA YANGAMrisho Ngassa Mtanzania anayechezea klabu ya Free State ya nchini Afrika Kusini amepongeza uwezo mkubwa waliouonyesha Yanga kwenye mechi yao dhidi ya MO Bejaia. Ngassa ambaye yupo likizo kwa sasa amesema Yanga walicheza vi… Read More
  • SAKATA LA KESSY YANGA HATIMA YAKE LEOSuala la beki wa Kulia wa Yanga, Hassan Ramadhan "Kessy" kucheza mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya TP Mazembe  itafahamika leo baada ya kamati ya utendaji Simba kukutana. Yanga iliwaandikia Simba barua kutaka kuj… Read More
  • MATUMAINI YA CANNAVARO KUELEKEA MCHEZO NA MAZEMBENahodha wa klabu ya Yanga, Nadir Haroub Cannavaro anaamini kuwa kikosi chao kitatinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho Barani (CAF CC). Yanga ambayo imepoteza mchezo wake wa kwanza kwa kukubali kipi… Read More

0 comments:

Post a Comment