Friday, May 27, 2016

ERICK MAWALLA AISHITAKI MBEYA CITY TFF

Shirikisho la Mpira Miguu nchini TFF, limepokea mashitaka kutoka kwa aliyekuwa mchezaji wa Mbeya City Erick Mawalla kwa kushindwa kumlipa pesa za usajili na mishahara zaidi ya Sh. milioni 10.



Mawalla amesema aliondolewa katika kikosi cha Mbeya City tangu mwaka jana baada ya aliyekuwa kocha wa City Meja Mingange kutokuwa na Mipango nae.

"Katibu (Emmanuel Kimbe) ndiye aliyenipigia simu kuwa sihitajiki kwenye timu, kocha hakuwa na mipango na mimi, niliomba nipewe barua lakini hakunipa zaidi ya kuniambia nitafute timu nyingine, kikubwa hata mshahara wangu nimeingiziwa kwa mara ya mwisho Oktoba mwaka jana. Hivyo nadai pesa ya Usajili na mishahara tangu kipindi hicho;" alisema Mawalla alipohojiwa na gazeti la Mwanaspoti.

Aidha Mawala amesema alishawaandikia barua ambayo kwa madai yake aliwapa muda wa wiki 2 wawe wamempa ufafanuzi juu ya mustakabali wake lakini hajajibiwa.Kutokana na hali hiyo na kutokupokelewa kwa simu zake anapowapigia viongozi wa Mbeya City ndipo Mawalla alipoamua kukimbilia TFF ili watoe mwongozo wa jambo hili ikiwezekana yeye apate haki yake.

Related Posts:

  • Dennis Kitambi Aeleza Siri Ya Ushindi Wao Dhidi Ya Majimaji KOCHA Msaidizi wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Dennis Kitambi, amesema kuwa maelekezo waliyowapa wachezaji wao ya kuongeza hali ya kupambana mchezoni kabla ya kuanza kipindi cha pili ndio yamepelekea… Read More
  • Yanga Yatinga Fainali Kombe La Shirikisho Coastal Union imepoteza mechi ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga baada ya washabiki wake kuwa chanzo cha Mwamuzi kuvunja mchezo huo uliofanyika Aprili 24, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Uam… Read More
  • TAIFA STARS KUCHEZA NA HARAMBEE STARS Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na timu ya Taifa Kenya (Harambee Stars) Mei 29, 2016 jijini Nairobi. Mche… Read More
  • SIMBA WAREJEA DAR TAYARI KWA KUIVAA AZAM FC TIMU ya Simba Sports Club imewasili jijini Dar wakitokea visiwani Zanzibar ambako walikwenda kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Azam FC. Simba inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi inahitaji ushindi katika mchez… Read More
  • Huyu Ndiye Afisa Habari Mpya TFF Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua Alfred Lucas kuwa Afisa Habari na Mawasiliano mpya wa shirikisho kuanzaia leo Aprili 27, 2016. Alfred anachukua nafasi ya Baraka Kizuguto aliyehamishiwa katika Kuruge… Read More

0 comments:

Post a Comment