Thursday, April 14, 2016

Tetesi Mpya Za Usajili Barani Ulaya Leo Alhamisi April 14,2016


Arsenal  Yamfukuzia Brozovic
Klabu ya Intermilan italazimika kumuuza nyota wake Marcelo Brozovic kwa ada ya Paundi Milioni 25 endapo itashindwa kufuzu kushiriki Michuano ya Klabu Bingwa Barani Ulaya Msimu Ujao. Arsenal imeonyesha nia ya kumtaka nyota huyo.

Source: Tuttosport

Thursday, April 14, 2016 02:16


Ibrahimovic Huenda Akaenda Qatar
Zlatan Ibrahimovic anaweza kuendelea kubaki Paris-Saint German kwa misimu mingine zaidi kabla hajaamua kukubali ofa nono ya kwenda kucheza soka nchini Qatar na kutupilia mbali Vilabu vya Ligi Kuu Uingereza vinavyomtolea macho.

Source: Sport

Thursday, April 14, 2016 02:13

West Brom Inamtaka Sakho Kuziba Pengo La Berahino
Klabu ya West Brom inataka kumsainisha Straika wa West Ham United Diafra Sakho kuchukua nafasi ya Saido Berahino ambae yupo mbioni kuondoka klabuni hapo. Sakho kapoteza nafasi yake West Ham ambao wanataka kumsainisha Jordan Ayew, Christian Benteke au Wilfred Bony.

Source: The Sun

Thursday, April 14, 2016 01:36

Man Utd Kuingia Katika Vita Na PSG Kumgombea Mourihno
Klabu ya Manchester United itapanda ushindani mkubwa kutoka kwa Matajiri wa Ufaransa Paris-Saint German kama PSG wataamua kumfukuza Kocha wao Laurent Blanc kufuatia kuondolewa kwao katika michuano ya Klabu Bingwa Ulaya.

Source: Daily Telegraph

Thursday, April 14, 2016 01:35

Juventus Inamwangalia Kwa Karibu Mshambuliaji Wa Liverpool Divock Origi
Klabu ya nchini Italia Juventus inaangalia uwezekano wa kumsajili Origi kutoka Liverpool  sambamba na Christian Benteke.

Source: Calciomercato.com

Wednesday, April 13, 2016 16:42

Oxlade-Chamberlain Ndio Chaguo Namba 1 La Southamton
Klabu ya Southampton inamwona Chamberlain kuwa ndo chaguo lao la kwanza, wamejiandaa kumfanya mchezaji huyo kuwa ni miongoni mwa wachezaji wanaolipwa zaidi  sambamba na kumpa ukapteni.

Source: Daily Mirror

Wednesday, April 13, 2016 01:51

Bale kutua Man Utd au Man City
Klabu ya Real Madrid ipo mbioni kumwongezea mkataba mnono Gareth Bale lakini mawakala wake wanafikiria kumrudisha Mchezaji huyo katika Ligi Kuu ya Nchini Uingereza Kujiunga Aidha na Manchester United au Manchester City.


Source: Tuttomercatoweb.com
Wednesday, April 13, 2016 01:46

Related Posts:

  • MATARAJIO YA SIMBA KIKOSI KIPYA MSIMU UJAOZacharia Hans Poppe, mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba, amesem a kikosi chao msimu ujao kitakuwa na mabadiliko makubwa kuanzia benchi la ufundi hadi wachezaji. Simba kwa sasa ipo katika harakati za kuhakikisha wanawana… Read More
  • HUYU NDO KOCHA MPYA BRAZILTite ametajwa kuwa kocha mpya wa Brazil baada ya Dunga kutupiwa virago kufuatia matokeo mabovu waliyoyapata Brazil Copa America 2016. Tite Tite 55, anachukua nfasi ya Dunga aliyetimuliwa mara baada ya Brazil kutolewa hatu… Read More
  • KIFAA KIPYA YANGA KUTUA LEO JANGWANIWalter Musona Mshambuliaji kutoka FC Platinum ya Zimbabwe anatarajiw kuwasili Daresalaam leo alasiri kwa ajili ya mazungumzo na klabu ya Yanga. Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka katika klabu ya Yanga, tayari mambo yo… Read More
  • KIFAA KIPYA CHAAHIDI MAKUBWA SIMBAKiungo mshambuliaji aliyesajiliwa na Simba hivi karibuni Jamali Mnyate amesema kusaini kwake Simba mkataba wa miaka 2 ni kujiendeleza kimpira na kuisaidia Simba kupata mataji. Mnyate aliyejiunga na Simba akitokea Mwadui F… Read More
  • RUVU SHOOTING KUKIPA NGUVU KIKOSI CHAORuvu Shooting ipo katika mipango ya kusajili wachezaji saba ili kujiimarisha kabla hawajaanza kipute cha ligi kuu Vodacom msimu wa 2016/17. kwa sasa Ruvu Shooting inaendelea na kambi kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwa… Read More

0 comments:

Post a Comment