Monday, April 11, 2016

Simba Katika Mtihani Mwingine Wa FA Leo Dhidi Ya Coastal Union

Timu ya Simba inajiandaa kupambana na Coastal Union ya Jijini Tanga leo Jumatatu katika Uwanja wa Taifa Dar es salaam, Kocha wa timu hiyo Jackson Mayanja amesema timu iko fiti wamejiandaa vizuri na wanatarajia ushindi katika mechi ya leo
.
Coastal na Simba zitamenyana kwenye mchezo wa Kombe la FA katika hatua ya robo fainali, wakiwa wanawania kuingia hatua ya nusu fainali huku timu za Yanga, Azam na Mwadui zikiwa tayari zimeshaingia katika hatua hiyo.

“Nimejiandaa vyema na kikosi changu kuelekea mechi yetu na Coastal, tunahitaji kushinda mchezo huo ili kuweza kufanikiwa kuingia hatua inayofuata
.

“Nashukuru wachezaji wangu wapo vyema na Kiiza na Juuko tayari wamesharejea kikosini na wanaendelea na mazoezi kwa ajili ya mchezo huo,” alisema Mayanja.

Related Posts:

  • MIPANGO YA JULIO KATIKA USAJILIKocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kiwelu "Julio" amesema yeye hana mpango wa kusajili wachezaji wa kigeni katika kikosi chake. Julio amesema lengo lake ni kutoa fursa kwa wachezaji wa ndani waweze kuonyesha uwezo wao ili waje ku… Read More
  • FARID MUSSA ASUBIRI RUHUSA YA AZAM FCFarid Mussa ni winga wa Azam FC aliyepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife ya nchini Hispania na kufanikiwa kufuzu majaribio hayo na sasa anasubiri ruhusa ya klabu tu ili aondoke zake. … Read More
  • BOCCO ATAJA KILICHOWAPONZA AZAM FCNahodha wa timu ya Azam FC, John Bocco amesema kuwa kushindwa kupata mafanikio katika msimu uliopita kumechangiwa na kuwakosa wachezaji wao muhimu katika kikosi hicho. Bocco alisema kukosekana kwa wachezaji muhimu katika k… Read More
  • KIPAUMBELE NAMBA 1 CHA SIMBA KATIKA USAJILI HIKI Simba ipo katika harakati za kuimarisha kikosi chao kwa kuhakikisha hawafanyi makosa katika usajili kipindi hiki ambacho dirisha la usajili limefunguliwa. Uongozi wa Simba umesema kipaumbele chao cha kwanza katika kipindi … Read More
  • KIWANGO KIBOVU CHA HAJI MWINYI CHAMUUMIZA PLUIJMKiwango cha beki wa kushoto wa Yanga Haji Mwinyi kinaonekana kushuka hali inayomfanya kocha Hans Pluijm kutafuta namna ya kulifanyia kazi suala hilo. Haji Mwinyi ni beki mwenye kipaji kikubwa anayeweza kuimudu vizuri nafas… Read More

0 comments:

Post a Comment