Mbrazil Neymar ni Mchezaji wa karibuni zaidi Mkataba wake kuvuja akiwa Barcelona baada ya Mtandao wa Football Leaks kuweka wazi mkataba wake mpya Camp Nou. Mchezaji huyo alihamia Barcelona akitokea Santos ya Nchini Brazil akisaini dili la miaka mitano mapema mwezi wa sita mwaka 2013 na baba yake akisemwa kuwa ndo mwakilishi wake katika dili hilo.
Mkataba huo unaonyesha thamani ya Mshahara ambao Neymar anapokea kwa mwaka ambao ni Euro milioni 5 achilia mbali bonasi mbalimbali zinazomfanya Mchezaji huyo wa kibrazil kujikusanyia zaidi ya Euro Million 49.5 katika kipindi chake chote cha Mkataba.
Neymar amekuwa na Mchango mkubwa sana katika klabu ya Barcelona akishirikiana vizuri na Messi na Suarez akiwa ameshafunga magoli 21 hadi sasa katika La Liga msimu wa 2015/2016.
Monday, April 11, 2016
Mkataba Wa Neymar Barcelona Wavuja
Related Posts:
POGBA ASHUSHWA OLD TRAFFORD KWA HELIKOPTA, MASHABIKI WACHACHAWAPicha Za Helikopta inayodhaniwa na mashabiki wa United kuwa ilikuwa imembeba Paul Pogba. Helikopta hiyo ilionekana kutua maeneo ya Old Trafford. Ungana na Soka24 Facebook, Bonyeza HAPA … Read More
VIDEO: CHEKI TIZI WANALOPIGA ATLETICO MADRID AUSTRALIA Tazama Video Hapa Chini Ungana na Soka24 Facebook, Bonyeza HAPA … Read More
RASMI: MANCHESTER CITY YAMNASA MORENO Klabu ya Manchester City iliyo chini ya kocha Mpya Pep Guardiola imekamilisha uhamisho wa kinda Mkolombia Marlos Moreno. Moreno 19, ametua katika dimba la Etihad akitokea Atletico Nocional na amesaini mkataba wa miaka mit… Read More
JAMES MILNER AACHANA NA TIMU YA TAIFA YA UINGEREZAJames Milner amestaafu kuitumikia timu yake ya taifa baada ya mazungumzo aliyofanya na Kocha mpya wa timu hiyo Sam Allardyce. Milner 30, anaachana na kikosi cha England akiwa ni mmoja kati ya wachezaji walioiwakilisha nchi… Read More
HII NDIO VIDEO INAYOMHUSISHA COSTA KUREJEA ATLETICO MADRID Tazama Video Hapa Chini Ungana na Soka24 Facebook, Bonyeza HAPA … Read More
0 comments:
Post a Comment