Monday, April 11, 2016

Niyonzima Arejea Na Kasi Mpya Yanga

Kiungo wao mchezeshaji Mnyarwanda, Haruna Niyonzima amepona malaria na tayari ameanza mazoezi.

Kiungo huyo, hivi karibuni alizuiwa kuingia kwenye kambi ya maandalizi huko Pemba katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly iliyochezwa juzi Jumamosi na matokeo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mnyarwanda huyo, pia aliukosa mchezo huo wa Al Ahly kutokana na adhabu ya kadi mbili za njano alizozipata katika mechi dhidi ya Cercle de Joachim ya Mauritius na APR ya Rwanda.

Niyonzima alisema juzi Jumamosi alianza mazoezi mepesi ya binafsi kwa kukimbia mbio ndefu na fupi kwa ajili ya kujiweka fiti.

Niyonzima alisema, amepanga kujiunga na wenzake katika mazoezi ya pamoja ya timu leo Jumatatu kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya Al Ahly itakayopigwa huko Misri.

“Mashabiki waondoe hofu na wanachotakiwa ni kuwa na matumaini makubwa ya kufanya vema katika mechi ijayo ya marudiano dhidi ya Al Ahly ambayo ninaamini tutapata matokeo mazuri.


“Mimi nimepona malaria, nashukuru nimeanza mazoezi mepesi ya binafsi kwa ajili ya kujiweka fiti zaidi baada ya kukaa nje ya uwanja kwa muda wa wiki moja, hivyo mechi ijayo nitakuwepo uwanjani,” alisema Niyonzima.

Related Posts:

  • KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA ESPERANCA KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA ESPERANCA 1. Deogratius Bonaventura Munishi. 2. Juma Abdul Japhary. 3. Oscar Fanuel Joshua. 4. Kelvin Patrick Yondani. 5. Nadir Haroub Ally. 6. Salum Abo Telela. 7. Saimon Happygod Msuva. 8… Read More
  • AZAM FC KUTUPA KARATA YAKE TENA DHIDI YA KAGERA SUGAR KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, inatarajia kuondoka kuelekea mkoani Mwanza kwa ajili ya kupambana na Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) utakaofanyika Uwanja wa Kambara… Read More
  • HIVI NDO VIINGILIO MECHI YA YANGA, ESPERANCA Uongozi wa Young Africans ya Dar es Salaam, umekamilisha maandalizi yote muhimu ya mchezo dhidi ya GD Sagrada Esperanca ya Angola wa kufuzu hatua ya makundi Kombe la Shirikisho la Barani Afrika utakaofanyika Uwanja wa Ta… Read More
  • FIFA YAILIMA FAINI SIMBA, YAPANGA KUISHUSHA DARAJA Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), limeipiga faini ya Franc 2,000 za Uswisi (sawa na Sh 4,582,000 za Tanzania), Klabu ya Simba baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kupuuza maagizo ya Idara ya Utatuzi wa Migogoro (Des… Read More
  • FAINALI FA CUP NA UWAKILISHI WA KIMATAIFA 2016/17 Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lingependa kutoa ufafanuzi kuwa iwapo Bingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa msimu 2015/16 inayoendelea atashinda pia taji katika fainali za Kombe la Shirikisho maarufu kama Aza… Read More

0 comments:

Post a Comment