Wednesday, April 13, 2016

Mwaka Wa Shetani Kwa Van Gaal, Ashusha Thamani Ya United Kifedha


Klabu ya Manchester United imejikuta ikishuka thamani yake  katika soka la hisa kwa zaidi ya paundi Milioni 400 katika msimu wa mwaka 2015/2016 kutokana na mwenendo mbovu wa klabu hiyo kwa sasa.
Kushuka huko kwa thamani kumechangiwa pia na kichapo cha hivi karibuni walichokipata mashetani wekundu hao kutoka kwa Tottenham Hotspurs.

Ripoti inaonyesha kwa kipindi cha miezi nane Manchester United imeshuka kutoka Paun za Uingereza Bilioni 2 hadi kufikia Paun Bilioni 1.58. Imekuwa ni bahati mbaya zaidi kwa kocha Louis Van Gaal kwani tangu anachukua timu mwaka 2014 thamani ya Manchester United katika soko la hisa ilikuwa ni Paun Milioni 650 kiwango kikubwa zaidi ukilinganisha na hali jinsi ilivyo kwa sasa.

Hali hiyo inayoikumba Manchester United kwa sasa imetokana pia na Kuondolewa kwao katika mashindano ya UEFA Champions League mwezi Disemba mwaka jana.

United wana  Mlima mrefu wa kuupanda kama wanataka kutetea nafasi yao katika Ligi Kuu Nchini Uingereza na kumaliza katika nafasi nne za juu. Kipigo cha 3-0 kutoka kwa Tottenham kimewaacha United pointi 4 nyuma ya Manchester City huku zikiwa zimebaki mechi sita tu kumaliza msimu.

Robo fainali ya FA wikendi hii huenda ikawapa United nafasi ya Kwenda Wembly endapo watafanikiwa kuwaondosha wagonga nyundo  West Ham United.

0 comments:

Post a Comment