Wednesday, April 13, 2016

Kwa Mchezo Huu Wakimataifa Wajitazame Upya.

Ligi ya vodacom imeendelea tena Leo katika viwanja viwili.
Mjini Morogoro Mtiwa Sugar waliikalibisha Azam Fc wakati Yanga ikicheza na Mwadui Fc ya Mjini Shinyanga katika uwanja wa taifa.

Azam Fc imecheza katika mazingira magumu ya uwanja wa Mtibwa uliokuwa umejaa Maji lakini walifanikiwa kuondoka na ushindi wa goli moja kwa bila dhidi ya Mtibwa Sugar, goli lililofungwa na John Bocco dakika ya 61' kwa mkwaju wa penati kufuatia rafu aliyochezewa mchezaji wa Azam katika eneo la hatari.

Katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Yanga imeibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja dhidi ya Mwadui Fc, Yanga imeonyesha kiwango kibovu sana ikizingatiwa kuwa inashiriki mashindano ya klabu bingwa na wanamchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahly April 19. Yanga wanatakiwa kuimarisha kikosi chao ili waweze kuleta ushindani mkubwa pale watakapoenda kucheza na Al Ahly.
Magoli ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva Dakika ya 13 na Harouna Niyonzima dakika ya 86.
Kwa matokeo hayo Yanga inafikisha pointi 56 ikiwa imeshacheza michezo 23 katika nafasi ya pili. Azam Fc nao kwa matokeo ya Leo wanafikisha pointi 55 katika nafasi ya tatu ikiwa imekwishacheza mechi 24 sawa na simba anaeshika nafasi ya kwanza kwa pointi 57.

Related Posts:

  • HIVI NDO VIKOSI VYA SIMBA NA AZAM FC LEO KIKOSI CHA SIMBA KIKOSI CHA AZAM FC 28 Aishi Manula 6 Erasto Nyoni 2 Gadiel Michael 13 Aggrey Morris 12 David Mwantika 16 Jean Mugiraneza 14 Ramadhan Singano 8 Salum Abubakar 10 Kipre Tchetche 19 John Bocco (C) 22 … Read More
  • SIMBA NA AZAM WAPELEKA SHANGWE JANGWANI MECHI ya Ligi kuu Bara kati ya Simba na Azam Fc imemalizika kwa timu hizo kutoka suluhu ya 0 - 0, Mchezo ulikuwa wa taratibu sana kipindi cha kwanza lakini kipindi cha pili hasa baada ya vurugu zilizotokea baada ya … Read More
  • BREAKING NEWS: AZAM FC YAPOKWA POINTI 3 NA MAGOLI 3 Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas, amesema katika mechi namba 156 iliyozikutanisha Mbeya City dhidi ya Azam kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya, Azam ilimchezesha Nyoni kinyume na … Read More
  • HAMISI TAMBWE AIFIKIA REKODI YA ABDALLAH JUMA YA MWAKA (2006) Mshambuliaji wa Klabu ya Yanga Hamisi Tambwe ndiye anaongoza katika chati ya ufungaji bora ligi Kuu Tanzania bara Msimu huu wa 2015/2016. Tambwe ambae jana alifunga goli katika mechi dhidi ya Stand United, alifikisha jum… Read More
  • AZAM FC YAZIDI KUISAFISHIA NJIA YANGA MCHEZO Wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa katika uwanja wa Chamanzi Complex leo, kati ya Azam FC na JKT Ruvu umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya 2 - 2. Matokeo hayo ya Sare yameifanya Klabu ya Azam FC kupoteza m… Read More

0 comments:

Post a Comment