Wednesday, March 1, 2017
Home »
Kitaifa
,
Matokeovpl
» Ruvu Shooting 0 - 2 Yanga SC , goli la Emanuel Marthin laacha gumzo Taifa
Ruvu Shooting 0 - 2 Yanga SC , goli la Emanuel Marthin laacha gumzo Taifa
Yanga waiadhibu Ruvu Shooting 2 - 1 uwanja wa Taifa.
kikosi cha yanga kikitoka kujeruhiwa na mnyama Simba leo katika dimba la uwanja wa Taifa jiji Dar es salaam wamekata ngebe za msemaji machachari wa Ruvu Masao Bwire.
Msemaji huyo alikaririwa na vyombo mbalimbali vya habari jana akitoa maneno makali na yenye msisimko pale aliposema "Yanga alishauliwa lakini hajazikwa hivyo kesho lazima tuzike".
ikiwa imefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi chake cha leo kwa kuwaanzisha Hassan Ramadhani Kessy, Nadir Haroub Canavaro, Vincent Bossou, . Deus Kaseke, Geoffrey Mwashuiya, iliwachukua dakika 30 ndipo walipopata penati baada ya mlinzi wa Ruvu kuunawa mpira uliopigwa na Obrey Chirwa.
mwamuzi aliamuru ipigwe penati na Saimon Msuva aliipa Yanga uongozi wa goli moja na goli lake la 12 msimu huu.
dakika ya 45 Obrey Chirwa alifunga goli safi kwa kichwa lakini Mwamuzi alilikataa goli hilo na kumpa kadi ya njano kabla ya 46' kumtoa nje kwa kosa la kumdharau mwamuzi.
Mpaka mapumziko mwenyeji Ruvu Shooting 0 - Yanga SC 1.
Kipindi cha pili Ruvu walikuja kwa nguvu na kukosa nafasi nyingi za wazi,
dakika ya 93 Emanuel Marthin alifunga goli saafi kwa kichwa baada ya krosi safi kutoka upande wa kulia iliyochongwa na Msuva.
mpaka mwisho wa mchezo Ruvu Shooting 0 - Yanga SC 2.
kwa matokeo hayo Yanga wamefikisha alama 52 katika michezo 23 wakiwa nafasi ya pili nyuma ya vinara Simba wenye 54 baada ya michezo 23.
Related Posts:
Ligi Daraja la kwanza Tanzania bara kuendelea leo february 11kwa michezo kadhaa kwa makundi miwili tofauti. Ligi Daraja la kwanza Tanzania bara kuendelea leo kwa michezo kadhaa kwa makundi miwili tofauti. KUNDI B: Mkoani Ruvuma Mlale JKT vs Kurugenzi FC Mkoani Njombe Njombe Mji vs Coastal Union KUNDI C: Mkoani… Read More
simba kukalia kiti cha uongoz wa ligi leo? ratiba kamili ya VPL Ligi kuu tanzania bara kuendela leo katika viwanja vinne, timu nane kumenyena kuwania taji la ligi kuu Tanzania bara (VPL). Michezo ya leo itazikutanisha timu ambazo zinataka kujinasua kutoka mkiani na timu ambazo zin… Read More
Rungu La TFF Latua Kwa Hemed Morocco Kamati ya Bodi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imemfungia Kocha wa Stand United, Hemed Morocco kushiriki michezo mitatu uwanjani na faini ya Sh 500,000. atika mechi Na. 160 ya Ligi Kuu ya Vodacom uliozikutanisha timu z… Read More
Manji Amcharukia Makonda Operesheni ya kuwataja hadharani wanaotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya limechukua sura mpya baada ya leo Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mh. Paul Makonda kutaja orodha ya awamu ya pili ambayo imewahusisha watu wengi … Read More
George Lwandamina Aifungukia Simba SC Kocha wa mabingwa soka Tanzania bara Timu ya Yanga Mzambia George Lwandamina ametamba kwamba mechi dhidi ya timu ya Ngaya Club ya Comoro katika mchezo wa klabu bingwa afrika zitawapa taswira nzuri kabla ya kuvaana na maasimu… Read More
0 comments:
Post a Comment