Wednesday, March 1, 2017
Home »
Kitaifa
,
Matokeovpl
» Ruvu Shooting 0 - 2 Yanga SC , goli la Emanuel Marthin laacha gumzo Taifa
Ruvu Shooting 0 - 2 Yanga SC , goli la Emanuel Marthin laacha gumzo Taifa
Yanga waiadhibu Ruvu Shooting 2 - 1 uwanja wa Taifa.
kikosi cha yanga kikitoka kujeruhiwa na mnyama Simba leo katika dimba la uwanja wa Taifa jiji Dar es salaam wamekata ngebe za msemaji machachari wa Ruvu Masao Bwire.
Msemaji huyo alikaririwa na vyombo mbalimbali vya habari jana akitoa maneno makali na yenye msisimko pale aliposema "Yanga alishauliwa lakini hajazikwa hivyo kesho lazima tuzike".
ikiwa imefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi chake cha leo kwa kuwaanzisha Hassan Ramadhani Kessy, Nadir Haroub Canavaro, Vincent Bossou, . Deus Kaseke, Geoffrey Mwashuiya, iliwachukua dakika 30 ndipo walipopata penati baada ya mlinzi wa Ruvu kuunawa mpira uliopigwa na Obrey Chirwa.
mwamuzi aliamuru ipigwe penati na Saimon Msuva aliipa Yanga uongozi wa goli moja na goli lake la 12 msimu huu.
dakika ya 45 Obrey Chirwa alifunga goli safi kwa kichwa lakini Mwamuzi alilikataa goli hilo na kumpa kadi ya njano kabla ya 46' kumtoa nje kwa kosa la kumdharau mwamuzi.
Mpaka mapumziko mwenyeji Ruvu Shooting 0 - Yanga SC 1.
Kipindi cha pili Ruvu walikuja kwa nguvu na kukosa nafasi nyingi za wazi,
dakika ya 93 Emanuel Marthin alifunga goli saafi kwa kichwa baada ya krosi safi kutoka upande wa kulia iliyochongwa na Msuva.
mpaka mwisho wa mchezo Ruvu Shooting 0 - Yanga SC 2.
kwa matokeo hayo Yanga wamefikisha alama 52 katika michezo 23 wakiwa nafasi ya pili nyuma ya vinara Simba wenye 54 baada ya michezo 23.
Related Posts:
Ruvu Shooting 0 - 2 Yanga SC , goli la Emanuel Marthin laacha gumzo Taifa Yanga waiadhibu Ruvu Shooting 2 - 1 uwanja wa Taifa. kikosi cha yanga kikitoka kujeruhiwa na mnyama Simba leo katika dimba la uwanja wa Taifa jiji Dar es salaam wamekata ngebe za msemaji machachari wa Ruvu Masao Bwire. M… Read More
Yanga Yaitwanga Mwadui, Yapaa Kileleni LIGI KUU TANZANIA BARA MZUNGUKO WA PILI RAUNDI YA 20 Yanga 2 - 0 Mwadui Chirwa 69', 83' Yanga Sasa inapanda katika nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara kwa kujikusanyia jumla ya alama 46 wakit… Read More
Matokeo Ligi Kuu Bara Matokeo Ligi Kuu Tanzania Bara Azam FC 2 - 0 Majimaji Young Africans 2 - 1 Mgambo JKT Simba SC 0 - 1 Toto Africans Young Africans 1 -… Read More
Mnyama Achinjwa Taifa Timu ya soka ya Simba imezidi kupoteza matumaini ya kunyakua ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kukubali kichapo cha Goli 1 - 0 toka kwa Toto Africans ya Mwanza.Katika mchezo huo ambao wadau wengi wa soka waliip… Read More
Simba yarudi kileleni, yaitumia salamu yanga february 25 Mpira ulianza kwa kasi na 11’ alimanusura Benjamin Asukile aifungie Prisons goli pale kichwa chake kilipoenda pembeni kidogo mwa lango la simba baada ya kazi nzuri ya Mohammed Samatta. Juma Luzio mchezaji wa Zesco Un… Read More
0 comments:
Post a Comment