Tuesday, January 10, 2017

simba yaitungua yanga bila huruma Zanzibar



Matuta yameamua mchezo wa yanga vs simba ndani ya uwanja wa amani.
Mchezo ulianza kwa kasi huku kila timu ikishambulia kwa tahadhari  kubwa na kujilinda kwa haraka.
Piga nikupige zilianza pale msuva alipokokota mpira kutoka lango la simba na kupiga mpira uliompita kipa wa simba lakini umakini wa beki za simba zilifanikiwa kuokoa hatari hiyo isiingie wavuni.
Dakika chache baadae Mohamed Ibrahim alipiga mkwaju mzito ulioguswa kwa ustadi mkubwa na kipa wa yanga Deo Munish na kugonga mlingoti wa juu ila umakini hafifu wa mshambuliaji wa simba ulisababisha apige hovyo na kuutoa nje mpira.
Mpka dakika 90 zinamalizika yanga 0 0 simba, kwa sharia za kombe la mapinduzi hatua ya nusu fainali mchezo ukiisha kwa sare kinachofuata ni mikwaju ya penati.
Simba ndio wa kwanza kupiga penati kupitia kwa nohodha wao Jonas Mkude ambae alipata, yanga alianza kipa wao DEogratius Munish lakini penati yake iliokolewa na kipa wa simba.
Penati ya pili ya simba alipiga golipa Agyei, wakati penati ya yanga ikipigwa na msuva  na wote walipata.
Penati ya tatu ya simba ilipigwa na Mwanjali akakosa wakati  kamusoko akapata.
Penati ya nne ya simba ilipigwa na mudhamiru akapata na upande wa yanga alipiga haji mwinyi akakosa.
Penati ya tano ya simba ilipigwa na mkongo Bokungu na kuiwezesha simba kupata ushindi wa goli 4 kwa 2.

Simba sasa itakutana na azam fainali siku ya ijumaa 13/1/ , azam wao walicheza mapema na kuifunga taifa jang’ombe goli 1 kwa 0, kwenye mchezo wa mapema.

0 comments:

Post a Comment