Monday, January 9, 2017

ni simba au yanga nusufainal Mapinduzi cup kesho



Tarehe 10/1/2017 mida ya saa mbili usiku katika dimba la uwanja wa Amani hatumwi mtu sokoni pale vinara wa kundi A simba sc itakapokutana na mahasimu wao wa jadi Yanga katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la Mapinduzi.
Huu utakuwa ni mchezo muhimu si tu kwamba ni nusufaili ya mapinduzi la hasha ni zaidi ya nusu fainali kwani simba na yanga ni wapinzani hata kwa mechi ya kirafiki, mara nyingi mchezo wa simba na yanga hautabiriki na
Kitu kizuri ni ujio wa makocha wawili wa simba na yanga , wawili hawa watakutana kwa mara ya kwanza katika historia ya timu zao, omog yeye kidogo anauzoefu wa kupambana na yanga akikinoa kikosi cha azam misimu michache iliyopita, lakini lwandamina yeye haijui simba ila ni mzoefu wa ligi mbali mbali za Afrika.
Yanga wapo na kumbukumbu ya kipigo cha aibu walichokipata toka kwa azam katika mchezo wake wa kukamilisha hatua ya makundi hivyo tutegemee mchezo ambao  yanga watajipanga kuwafurahisha washabiki wao.
Simba wao wanataka matokeo chanya ili kuondoa uteja ambao umeonekana kuanza kuota mizizi kwa kipindi hiki cha miaka miwili.
Hitimisho atakaemzidi mwenzie mbinu ndio mshindi wa mchezo huo muhimu.

Mchezo mwingine wa mapema ni kati ya azam na jong’ombe boys kutoka visiwani Zanzibar majira ya saa kumi jioni.


0 comments:

Post a Comment