Tuesday, August 30, 2016

SIMBA YABADILI GIA ANGANI

Sare ya bila kufunguna waliyoipata Simba dhidi ya JKT Ruvu imemfanya kocha wa klabu hiyo, Joseph Omog kubadili mfumo wa uchezaji na kusisitiza umakini kwa wachezaji katika mechi zijazo.

Katika mchezo huo dhidi ya JKT Ruvu Simba ilionyesha kandanda safi sana licha ya kutofanikiwa kupata goli. Kufuatia matokeo hayo Mcameroon huyo amesema analazimika kubadili aina ya uchezaji (Mfumo) kwa kucheza kwa malengo huku wakitafuta njia za kufunga mabao pale wanapokuwa na mchezo mgumu kama ambavyo ilikuwa kwa JKT Ruvu.

“Tulicheza vizuri lakini hatukupata ushindi siyo matokeo mabaya, lakini pia siyo mazuri kwa sababu ligi ina ushindani unapopata matokeo tofauti na ushindi inakuwa mbaya na sasa nimeona tubadili mfumo wa uchezaji wetu tuache kupiga pasi nyingi na sasa tunatakiwa kwenda mbele kutafuta ushindi na kila mchezaji wangu nataka aongeze umakini awapo uwanjani,” alisema Omog.

Aidha Omog aliongeza kuwa, pamoja na kwamba matokeo hayo ya sare siyo mabaya lakini yeye kama kocha hayajamfurahisha na ndio sababu ya kupanga kubadilisha mfumo katika kikosi chake.
Kocha huyo pia amewataka mashabiki wa Simba watulie na kuondoka shaka kwa matokeo hayo ya sare kwani ligi ndo inaanza huku akisisitiza kwamba kuna safari ndefu hadi kufikia mwisho wa kumpata bingwa.

=============
Stori Kubwa Zinazotikisa Anga La Michezo Hivi Sasa;
Aubameyang Aitamani Real Madrid

Nyota Wa Zamani Wa Man U Aitabiria Ubingwa Chelsea


Omog Ashusha Presha Za Wana Msimbazi


"Yanga Timu Bora Zaidi Tanzania" Pluijm

Ungana na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA


Related Posts:

  • AARON NYANDA AJIENGUA UCHAGUZI YANGA Nyanda aliyekuwa anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Yanga, amejitoa kushiriki uchaguzi huo utakaofanyika kesho Juni 11, 2016. Nyanda ambaye alichukua fomu za kuwania nafasi hiyo kwenye ofisi za shirikisho la mpira w… Read More
  • YANGA YATUMA MAJINA YA NYOTA WAO WAPYA CAFKlabu ya Yanga imewasilisha majina ya wachezaji wake CAF waliowasajili hivi karibuni ambao ni Hassan Ramadhan Kessy, Juma Mahadhi, Vicent Andrew na Beno Kakolanya kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo katika kombe la shirikisho … Read More
  • MTIBWA HAITAMBUI USAJILI WA ANDREW VICENT YANGA Klabu ya Yanga hivi karibuni ilitangaza kumnasa mchezaji wa Mtibwa Sugar Andrew Vicent "Dante" lakini Msemaji wa Klabu ya Mtibwa, Thobias Kifaru amesema hana taarifa hizo. Klabu ya Mtibwa Sugar imesema haijapata taarifa j… Read More
  • YANGA KUANZA KAMBI RASMI LEO Timu ya Dar Young Africans inatarajiwa kuingia kambini leo kujiandaa na michezo ya hatua ya makundi CAF Confederation Cup. Yanga itacheza mchezo wake wa kwanza katika hatua hiyo Juni 19 dhidi ya MO Bejaia ya nchini Algeri… Read More
  • SIMBA YAMNASA WINGA MACHACHARI, ASAINI MIAKA 2 Klabu ya Simba Sports Club imefanikiwa kumsajili mchezaji wa Mwadui FC, Jamali Mnyate aliyesaini mkataba wa miaka 2 kwa uhamisho wa Tsh. Milioni 15. Kufuatia usajili huo Makamu Rais wa klabu hiyo, Geofrey Nyange Kaburu a… Read More

0 comments:

Post a Comment