Sunday, August 14, 2016

KAULI ZA MAKOCHA YANGA,MO BEJAIA BAADA YA MECHI JANA

Mchezo kati ya Yanga na MO Bejaia jana umemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa goli moja kwa sufuri.
Matokeo hayo yamefufua matumaini ya Yanga kuwania kucheza hatua ya Nusu fainali kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF CC), hata hivyo matumaini hayo yanategema matokeo ya mchezo wa leo kati ya Medeama dhidi ya MO Bejaia, na dua za Wanayanga wengi leo ni kuiombea ushindi klabu ya TP Mazembe huku wao wakitakiwa kuifunga TP Mazembe katika mchezo wao wa Mwisho wakati huo pia mchezo kati ya MO Bejaia na Medeama watoe Sare.

Baada ya kumalizika mchezo wa Jana, makocha wa timu zote Mbili waliyasema yafuatayo;

"Mwanzo tulikuwa tunauoga Kidogo, lakini kipindi cha pili tulitulia na kutengeneza nafasi nyingi, Kwa Bahati Mbaya hatukuweza kuzitumia nafasi hizo, Sasa hivi tunasubiri matokeo ya mechi kati ya Medeama-Mazembe tuone kama bado tutakuwa na nafasi ya kufuzu, lakini vyovyote itakavyokuwa tutapambana na kushinda mechi ya mwisho" Alisema Kocha Wa Yanga, Hans Van Pluijm Baada ya Kumalizika kwa mchezo wa jana.

"Tuliuchukulia mchezo kwa Umakini Mkubwa sana, Kwa Bahati mbaya hatujashinda. Mipango yetu imevurugwa kwa sasa na tunatakiwa kupambana kwa nguvu zetu zote kushinda katika mchezo wetu wa Mwisho" alisema Nasser Sandjak Kocha Mkuu wa timu ya MO Bejaia jana baada ya kumalizika kwa mchezo wa Jana.
Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA 

Related Posts:

  • CAF YAIFUTA ES SETIF KLABU BINGWA AFRIKAMabingwa mara mbili wa kombe la klabu bingwa Afrika, ES Setif wametolewa katika michuano hiyo kufuatia vurugu zilizofanywa na mashabiki wao. Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limeiondoa klabu ya ES Setif kweny… Read More
  • CAF YAIBEBA YANGA KUELEKEA MECHI NA MAZEMBEShirikisho la Mpira wa miguu barani Afrika CAF, limewaidhinisha wachezaji watatu wa Yanga ambao walikuwa wanatumikia adhabu ya kadi kucheza, kucheza katika mchezo wao na TP Mazembe. Wachezaji wa Yanga, Oscar Joshua, Nadir … Read More
  • KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA MO BEJAIA CAF CC KOMBE LA SHIRIKISHO BARANI AFRIKA (CAF CC)KUNDI A. MO Bejaia (Algeria) Vs Young African SC (Tanzania). Uwanja :- Unite Maghrebine. Muda :-Saa 6 : 15 Usiku (Tanzania). KIKOSI CHA YANGA LEO. 1: Deogratius Munishi 'Dida' 2… Read More
  • HII NDO HALI ILIYOPO UWANJA WA TAIFA WATU WAMEFURIKA Kuelekea Mchezo kati ya Yanga na TP Mazembe Leo Jioni Hivi Ndivyo Mashabiki Walivyofurika Uwanja Wa Taifa Mapema Leo Kusubiri Mchezo Huo. KILA LA KHERI YOUNG AFRICA Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa … Read More
  • YANGA YAANZA VIBAYA HATUA YA MAKUNDI CAF CCMchezo wa kombe la shirikisho Afrika CAF hatua ya makundi kati ya MO Bejaia na Yanga umamalizika kwa Yanga kukubali kichapo cha goli 1 kwa bila, goli lililofungwa na Yassine Salhi dakika ya 20' ya Mchezo. Kwa matokeo hayo Ya… Read More

0 comments:

Post a Comment