Friday, August 5, 2016

JAMES MILNER AACHANA NA TIMU YA TAIFA YA UINGEREZA

James Milner amestaafu kuitumikia timu yake ya taifa baada ya mazungumzo aliyofanya na Kocha mpya wa timu hiyo Sam Allardyce.

Milner 30, anaachana na kikosi cha England akiwa ni mmoja kati ya wachezaji walioiwakilisha nchi hiyo katika michuano minne mikubwa ikiwemo Euro 2016 iliyomalizika hivi karibuni huko nchini Ufaransa.

Kiungo huyo wa Liverpool ametoa nafasi kwa kizazi kipya kutoa mchango wao katika kikosi hicho cha England na tayari Shirikisho la mpira wa miguu nchini humo limetangaza uamuzi huo wa Milner leo Ijumaa Agosti 5,2016.

"Napenda kutoa shukrani zangu kwa Sam kwa kukutana na mimi na kulizungumzia suala langu na hatimaye kufikia makubaliano" alisema Milner.

"Nadhani maamuzi tuliyoyafikia ni kwa lengo zuri tu kwa taifa. Namtakia Sam, Wachezaji, Viongozi wote pamoja na mashabiki mafanikio mema hapo mbeleni" aliongeza Mkongwe huyo anayekipiga katika klabu ya Liverpool.
Ungana na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA 

Related Posts:

  • SPURS NA ARSENAL KUWANIA SAINI YA MIDFIELD RAIA WA KENYA Tottenham Na Arsenal Wanasaka Saini Ya Midfieda Wa Southampton Victor Wanyama Wanyama alikuwa karibu kujiunga na Tottenham msimu uliopita lakini dili hilo lilifeli. Inasemekana Spurs bado wanania ya kumsajili Wanyama w… Read More
  • HUYU NDO ALIYEIFUNGISHA LIVERPOOL KWENYE FAINALI EUROPA Liverpool imepoteza mchezo wake wa fainali dhidi ya Sevilla kwa kufungwa magoli 3 - 1 na Alberto Moreno ndo ameonekana kuiangusha timu. Liverpool imepoteza katika mchezo wake wa fainali kombe la Europa jana baada ya ku… Read More
  • MASHABIKI 17 WA LIVERPOOL WATIWA NDANI Mashabiki 17 wa Liverpool walitiwa kizuizini na kuachiwa kufuatia matukio yaliyojitokea katika mchezo wa fainali Europa League Jana. Police wa Basel waliwakamata mashabiki 30 na kuwaweka ndani 17 wakiwa ni wa Liverpo… Read More
  • RAIS WA CAF ATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI CAMEROON Rais wa shirikisho la Mpira wa miguu barani Africa Issa Hayatou ametuma salam za rambirambi Cameroon kufuatia kifo cha David Mayebi katika barua ya tarehe 18 Mei 2016 iliyotumwa kwa rais wa shirikisho la mpira wa migu… Read More
  • SERENGETI BOYS YATINGA NUSU FAINALI Timu ya soka ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ leo Mei 19, 2016 imetinga hatua ya Nusu Fainali baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Korea Kusini  Timu ya soka ya Taifa ya Vijana wen… Read More

0 comments:

Post a Comment