Thursday, August 11, 2016

DAVID MOYES AWANASA WAWILI KUTOKA MANCHESTER UNITED

Boss Mpya wa klabu ya Sunderland, David Moyes amekamilisha usajili wa wachezaji wawili kutoka katika klabu ya Manchester United.

Klabu ya Manchester United imethibitisha kuuzwa kwa wachezaji wao wawili ambao ni Paddy McNair na Donald Love waliojiunga na klabu ya Sunderland kwa jumla ya ada ya uhamisho ya pauni 5.5 kwa wachezaji wote wawili.

Wawili hao wameenda kuungana na kocha wao wa zamani David Moyes na tayari usajili huo umeshakamilika na kuthibitishwa na klabu zote mbili.

McNair 21, alijiunga na Manchester United mwaka 2011 baada ya kuonwa na mascouti wa klabu hiyo lakini hakuwahi kucheza hadi Van Gaal alipoichukua timu na kwa mara ya kwanza akaichezea United katika msimu huo.

Akizungumzia usajili huyo Moyes amesema analengo la kuongeza wachezaji makinda kwenye kikosi chake pamoja na wakongwe ili kwa umoja wao waweze kuleta matunda katika kikosi hicho.

"Nataka kuongeza wachezaji makinda kwenye kikosi pamoja na wakongwe. Nataka niwalete wachezaji ambao watakuwepo hapa (klabuni) kwa muda mrefu na muda mfupi na natumai hawa wawili watakuwepo kikosini kwa muda mrefu"

Related Posts:

  • MAISHA YA FABREGAS CHELSEA YAFIKA UKINGONI Cesc Fabregas ameambiwa na kocha wa klabu ya Chelsea Antonio Conte kuwa anaweza kuondoka klabuni hapo. Conte ametoa kauli hiyo huku kukiwa kumebaki siku 2 tu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya. Kiungo h… Read More
  • AUBAMEYANG AITAMANI REAL MADRID Hakuna ubishi kuwa Nyota wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang anatamani kujiunga na miamba ya soka ya nchini Hispania klabu ya Real Madrid. Aubameyang amewahi kumuahidi babu yake kuwa ipo siku atakuja kucheza k… Read More
  • WEST BROM YAVUNJA REKODI YA KLABU USAJILI WA CHADLI Klabu ya West Bromwich Albion imevunja rekodi ya klabu hiyo kwa kumsajili Winga wa Tottenham Spurs kwa kitita cha Pauni milioni 13. Chadli alijiunga na Spurs akitokea FC Twente kwa uhamisho wa pauni milioni 7 Julai 2013… Read More
  • Rasmi: Wilfred Bony Atua Stoke City Klabu ya Stoke City imekamilisha uhamisho wa Wilfred Bony kwa mkopo akitokea klabu ya Manchester City. Bony aliyefeli kumshawishi kocha mpya wa City, Mhispania Pep Guardiola amefanikiwa kufunga magoli 11 katika michezo 4… Read More
  • WALIOSAJILIWA,WALIOACHWA MAN U MSIMU WA 2016-17 Kuelekea Msimu wa 2016-17 klabu ya Manchester United imekamilisha Usajili Ufuatao; WALIOINGIA; MCHEZAJI KLABU ALIYOTOKA ADA YA UHAMISHO Eric Bailly … Read More

0 comments:

Post a Comment